TAJIRI AMCHOMA MOTO KIJANA NA KUMKATA KATA /POLISI WANYAMAZISHAWA /AMTELEKEZA HOSPITAL YA MT MERU

 

Kijana Prims Eliaringa (22), mkazi wa mtaa wa Siara, kata ya Baraa jijini Arusha, amedai kushambuliwa kwa kuchomwa moto na kukatwa mapanga na mtu mmoja anayedaiwa kuwa tajiri, aitwaye Donald Mola, pamoja na mafundi wa ujenzi.

Tukio hilo linadaiwa kutokea Machi 28, 2025, wakati kijana huyo alipokuwa akielekea kuomba kazi ya kusaidia mafundi katika nyumba inayojengwa eneo hilo.

Kwa mujibu wa maelezo ya Prims, alipofika kwenye eneo la ujenzi, alikamatwa na mafundi hao, akatuhumiwa kuwa mwizi na kuanza kushambuliwa bila kufanyiwa mahojiano yoyote. Anadai alikatwa mapanga na kuchomwa moto katika sehemu mbalimbali za mwili wake.

Baada ya kushambuliwa, alifungwa kamba na kuwekwa kwenye buti ya gari. Alidai kusafirishwa hadi kwa mwenyekiti wa mtaa, kisha kwa polisi, na baadaye kutupwa katika hospitali ya Mount Meru kwa ajili ya matibabu.

Mama mzazi wa kijana huyo, Bi. Rahel Joseph, amesema licha ya kufunguliwa jalada la kesi lenye kumbukumbu namba ARS/RB/3075/2025, mtuhumiwa hajachukuliwa hatua yoyote. Anadai kuwa Donald Mola anatumia ushawishi wake wa kifedha kukwepa mkono wa sheria.

Mwenyekiti wa mtaa huo, James Daniel, amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kueleza kuwa alimpokea Prims akiwa katika hali mbaya. Ameonya wananchi kuacha kujichukulia sheria mikononi.

Juhudi za kumpata Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Arusha, Justin Masejo, hazikufanikiwa baada ya simu yake kuita bila kupokelewa.

TAJIRI AMCHOMA MOTO KIJANA NA KUMKATA KATA /POLISI WANYAMAZISHAWA /AMTELEKEZA HOSPITAL YA MT MERU TAJIRI AMCHOMA MOTO KIJANA NA KUMKATA KATA /POLISI WANYAMAZISHAWA /AMTELEKEZA HOSPITAL YA MT MERU Reviewed by KUSAGANEWS on April 21, 2025 Rating: 5

No comments: