DK NCHIMBI ;MBOWE ,MNYIKA HAWAHUSIKI SAKATA LA KIBAO ,UCHUNGUZI UHARAKISHWE.















Katibu Mkuu  wa CCM ,Dk Emmanuel Nchimbi  amesema chama hicho kimeanza mazungumzo yasiyo  rasmi na vyama vya Upinzani vikiwemo Chadema na ACT -Wazalendo .


Dk  Nchimbi amesema hayo leo Ijumaa,Septemba 13,2024 ofisi ndogo za CCM ,Lumumba  jijini Dar es Salaam wakati akizungumza na wahariri na waandishi wa habari .


Mtendaji mkuu huyo amesema hayo yote wakati akijibu swali aliloulizwa juu ya umuhimu wa mazungumzo baina ya CCM na vyama vingi ili kudumisha kuaminiana na amani ya nchi.


Amesema kuna mazungumzo yasiyo rasmi yanayoendelea na anafanya yeye mwenywe kwa lengo la kupata mwafaka wa Taifa .


Dk Nchimbi amesema hata washiriki wa mazungumzo hayo nupande wa CCM watachagua wale wenye nia na lengo zuri la mazungumzo  kwani baadhi 'Ukiwaona tu anavyozungumza  unaona huyu hafai ,tutachagua wenye engo la maridhiano'.


'Kwa upande wetu ,tutafanya kila linalowezekana kuhakikisha mazungumzo yanakuwepo'amesema Dk Nchimbi.

DK NCHIMBI ;MBOWE ,MNYIKA HAWAHUSIKI SAKATA LA KIBAO ,UCHUNGUZI UHARAKISHWE. DK NCHIMBI ;MBOWE ,MNYIKA  HAWAHUSIKI SAKATA LA KIBAO ,UCHUNGUZI UHARAKISHWE. Reviewed by KUSAGANEWS on September 13, 2024 Rating: 5

No comments: