Mwanamke aitwae Neema Kabulu (19)
amenusurika kufa baada ya kukatwa na kitu chenye ncha kali sehemu za usoni,
tumboni,mkononi na Mwalimu Joseph Msafiri wa Shule ya Msingi Namagubu iliyoko
Ukerewe Mkoani Mwanza ambaye ni mpenzi wake.
Kwa Mujibu wa taarifa ya Kamanda wa
polisi mkoa wa Shinyanga,ACP Richard Abwao kwa vyombo vya habari,tukio hilo
limetokea Septemba 6,2019 majira ya saa nne kamili usiku katika maeneo ya Old
Shinyanga, Kata ya Old Shinyanga, Tarafa ya Shinyanga Mjini, Manispaa ya
Shinyanga.
"Neema
Kabulu mkazi wa Ukerewe mkoani Mwanza alijeruhiwa kwa kukatwa na kitu chenye
ncha kali sehemu za usoni, tumboni na mkono wa kulia na Joseph Msafiri ambaye
ni Mwalimu wa Shule ya Msingi Namagubu iliyoko ukerewe Mkoani Mwanza, ambaye ni
mpenzi wake",ameeleza Kamanda Abwao.
"Chanzo
cha tukio hilo ni wivu wa kimapenzi. Majeruhi anapatiwa matibabu katika
Hospitali ya Rufaa Mkoa wa Shinyanga na hali yake ni mbaya. Mtuhumiwa
amekamatwa",ameongeza.
Mwalimu wa shule ya msingi mbaroni kwa kuchoma tumbo la mpenzi wake shinyanga
Reviewed by KUSAGANEWS
on
September 08, 2019
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
September 08, 2019
Rating:


No comments:
Post a Comment