Umoja wa vijana (UVCCM) wilayani Arumeru imezindua
Lemanyata ya Kijani na kutoa pongezi kwa umoja huo na Chama kata ya Lemanyata
kwa kazi kubwa inayofanywa katika Kata hiyo.
Mgeni rasmi ambaye ni Katibu wa Jumuiya hiyo ya Vijana
(UVCCM) wilaya ndugu Hussein Manipula katika uzinduzi huo wa Lemenyata ya
Kijana , ametoa pongezi nyingi sana za ujenzi wa kivuko kinachounganisha Kijiji
cha Lemanyata na Mtaa wa Seuri.
Awali katika ukaguzi wa kivuko hicho, Katibu wa CCM Kata
ya Lemanyata ndugu Samwel Kikois amesema kivuko hicho hadi sasa kimegharimu
mnamo shilingi M 6 huku sehemu
iliyobaki kikitazamiwa kugharimu milioni 4 huku akisema fedha hizo zilizotumika
ni michango kutoka kwa wananchi wa vijiji hivyo na mchango kutoa kwa Mkurugenzi
Wilaya.
Sambamba na zoezi la ukaguzi wa kivuko hicho, uzinduzi
wa Kijani kata ya Lemanyata ulifanyika na kuhudhuriwa na vijana kutoka katika
vijiji vinavyounda kata hii ya Lemanyata.
Aidha UVCCM kata ya Lemanya katika risala yao waliomba
Jumuiya hiyo UVCCM na Chama Cha Mapinduzi (CCM) wapatiwe Elimu ya Ujasiriamali
na upatikanaji wa vifaa vya michezo.
Aidha Mgeni Rasmi Ndugu Hussein Manipula amesema kuwa
Serikali imeandaa mpango mkakati wa kuhakikisha Vijana wanapata Elimu ya
Ujasiriamali bila ubaguzi.
Hata hivyo Manipula amewataka Vijana na wananchi kwa
ujumla kuhakikisha katika chaguzi zijazo wafanye uchaguzi wa kuwachagua
viongozi bora na siyo bora viongozi.
Nayo UVCCM kata ya Lemanyata kimempokea aliyekuwa Katibu
wa BAVITA Lemanyata ndugu Osotwa Kisambu na wanachama vijana wengine zaidi ya
100 kukabidhiwa kadi za Jumuiya hiyo.
Vijana hao waliorudisha kadi zao na kupokea kadi za
UVCCM walikula kiapo cha utii kwa CCM
mbele ya Hamasa Wilaya ndugu Nicholas Sawa.
Zoezi hilo la uzinduzi wa Lemanyata ya Kijani limeenda
sambamba na kutoa zawadi kwa timu tatu za michezo zilicheza mpira wa miguu
zilizofanya vizuri katika michuano yao zilizokuwa zikicheza ligi katika kata
hiyo ya Lemanyata.
Arumeru wazindua Lemanyata ya Kijani ,Vijana wahimizwa chaguzi zijazo
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 31, 2019
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 31, 2019
Rating:


No comments:
Post a Comment