Arumeru wazindua Lemanyata ya Kijani ,Vijana wahimizwa chaguzi zijazo


Umoja wa vijana (UVCCM) wilayani Arumeru imezindua Lemanyata ya Kijani na kutoa pongezi kwa umoja huo na Chama kata ya Lemanyata kwa kazi kubwa inayofanywa katika Kata hiyo.

Mgeni rasmi ambaye ni Katibu wa Jumuiya hiyo ya Vijana (UVCCM) wilaya ndugu Hussein Manipula katika uzinduzi huo wa Lemenyata ya Kijana , ametoa pongezi nyingi sana za ujenzi wa kivuko kinachounganisha Kijiji cha Lemanyata na Mtaa wa Seuri.

Awali katika ukaguzi wa kivuko hicho, Katibu wa CCM Kata ya Lemanyata ndugu Samwel Kikois amesema kivuko hicho hadi sasa kimegharimu mnamo shilingi M 6 huku   sehemu iliyobaki kikitazamiwa kugharimu milioni 4 huku akisema fedha hizo zilizotumika ni michango kutoka kwa wananchi wa vijiji hivyo na mchango kutoa kwa Mkurugenzi Wilaya.

Sambamba na zoezi la ukaguzi wa kivuko hicho, uzinduzi wa Kijani kata ya Lemanyata ulifanyika na kuhudhuriwa na vijana kutoka katika vijiji vinavyounda kata hii ya Lemanyata.

Aidha UVCCM kata ya Lemanya katika risala yao waliomba Jumuiya hiyo UVCCM na Chama Cha Mapinduzi (CCM) wapatiwe Elimu ya Ujasiriamali na upatikanaji wa vifaa vya michezo.

Aidha Mgeni Rasmi Ndugu Hussein Manipula  amesema kuwa  Serikali imeandaa mpango mkakati wa kuhakikisha Vijana wanapata Elimu ya Ujasiriamali bila ubaguzi.

Hata hivyo Manipula amewataka Vijana na wananchi kwa ujumla kuhakikisha katika chaguzi zijazo wafanye uchaguzi wa kuwachagua viongozi bora na siyo bora viongozi.

Nayo UVCCM kata ya Lemanyata kimempokea aliyekuwa Katibu wa BAVITA Lemanyata ndugu Osotwa Kisambu na wanachama vijana wengine zaidi ya 100 kukabidhiwa kadi za Jumuiya hiyo.

Vijana hao waliorudisha kadi zao na kupokea kadi za UVCCM walikula kiapo  cha utii kwa CCM mbele ya Hamasa Wilaya ndugu Nicholas Sawa. 

Zoezi hilo la uzinduzi wa Lemanyata ya Kijani limeenda sambamba na kutoa zawadi kwa timu tatu za michezo zilicheza mpira wa miguu zilizofanya vizuri katika michuano yao zilizokuwa zikicheza ligi katika kata hiyo ya Lemanyata.
Arumeru wazindua Lemanyata ya Kijani ,Vijana wahimizwa chaguzi zijazo Arumeru wazindua Lemanyata ya Kijani ,Vijana wahimizwa chaguzi zijazo Reviewed by KUSAGANEWS on August 31, 2019 Rating: 5

No comments: