Mahakama ya Rufani imetupilia mbali
ombi la kuangaliwa upya hukumu ya kunyongwa, aliyohukumiwa Christopher Bageni,
ambaye alifungua shauri hilo kutaka afutiwe adhabu hiyo, kwa kosa la mauaji ya
wafanyabiashara watatu wa madini mkoani Morogoro.
Uamuzi wa kutupilia mbali maombi
hayo ya Bageni ulioandaliwa na jopo la majaji watatu wa mahakama hiyo
waliosikiliza maombi hayo, umetolewa leo Jumatano, Agosti 14, 2019 na Naibu
Msajili Mwandamizi wa Mahakama ya Rufani, Elizabeth Mkwizu.
Jopo la majaji hao waliosikiliza na
kutoa uamuzi wa maombi hayo namba 63 ya mwaka 2016 ni Stella Mugasha
(kiongozi), Ferdinarnd Wambali na Rehema Kerefu.
Kutokana na uamuzi huo wa Mahakama,
Bageni hana namna nyingine ya kukata rufaa wala kutafuta namna nyingine ya
kisheria kwani hakuna ngazi nyingine ya mahakama nchini wala hatua nyingine
ambayo anaweza kuichukua.
Kwa sasa atasubiri tu utekelezaji
wake huku akiombea neema ya rais wa awamu ya sasa au awamu zijazo kumsamehe ama
kumwachia huru au kumbadilishia adhabu pengine kuwa ya kifungo kwa mamlaka yake
kikatiba kama ataguswa au kuona kuna sababu ya kufanya hivyo.
Rufaa ya Mrakibu wa Polisi Kupinga Hukumu ya Kunyongwa Yatupiliwa Mbali
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 14, 2019
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 14, 2019
Rating:


No comments:
Post a Comment