Dereva afukuzwa kazi kwa kumruhusu nyani aendeshe basi la abiria

Dereva wa basi la abiria nchini India amefukuzwa kazi baada ya kumruhusu nyani aendeshe basi hilo

Dereva huyo amefukuzwa ingawa hakuna hata abiria mmoja aliyekuwa kwenye basi hilo ambaye alilalamikia kitendo cha dereva huyo kumruhusu nyani kuendesha basi hilo

Hata hivyo baada video ya nyani huyo aliyekuwa ametulia huku akiwa ameshikilia usukani wa basi hilo kusambaa mitandaoni, waajiri wake walimchukulia hatua ya kumfukuza

Hata hivyo hatua hiyo ya waajiri kumfukuza kazi dereva huyo haijawafurahisha watumiaji wa mitandao ambao walifurahishwa na video hiyo

"Vizuri sana, kwa nini mumfukuze . Angepewa onyo na aambiwe asirudie, mmoja wa wasomaji aliandika katika ukurasa wake wa Twitter

Kwa mujibu wa walioshuhudia, nyani alipanda gari na abiria mwingine lakini akakataa kukaa nyuma bali akachagua kiti cha dereva

Dereva huyo aliyefahamika kwa jina la Prakash, ambaye alionekana kutotilia maanani sana suala hilo, alimruhusu nyani kukaa kwenye usukani huku wakiendelea na safari

Inadaiwa kwamba nyani huyo alipofika kwenye kituo chake alishuka na kumuacha dereva akiendelea na safari yake.



Dereva afukuzwa kazi kwa kumruhusu nyani aendeshe basi la abiria Dereva afukuzwa kazi kwa kumruhusu nyani aendeshe basi la abiria Reviewed by KUSAGANEWS on October 07, 2018 Rating: 5

No comments: