Mkazi wa kijiji cha Makunduchi
mkoani Kusini Unguja, Zuwena Haji Mwadini (14) amefariki kwa kujinyonga kwa
kutumia mtandio.
Kamanda wa polisi mkoa wa Kusini
Unguja, Suleiman Hassan Suleiman alisema kwamba tukio hilo lilitokea Agosti 17.
Alisema binti huyo alikuwa
mwanafunzi wa darasa la sita na kwamba, sababu za kujinyonga ni ugomvi baina
yake na mdogo wake.
Suleiman alisema tofati baina ya
watoto hao ilisababisha kuchukua uamuzi huo na kuongeza kuwa tukio hilo si la
kawaida.
Pia, Suleiman aliwataka vijana
kuacha kuchukua uamuzi wa haraka.
Mwanafunzi Darasa la 6 Ajinyonga kwa Mtandio
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 20, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment