Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji imesema
itahakikisha amani inakuwapo ili kuwavutia wawekezaji wengi.
Naibu Waziri wa
wizara hiyo, Mhandisi Stella Manyanya amesema, “Amani ni jambo la msingi na
sisi tutalifanyia kazi. Lakini amani ianze humu bungeni na kwa kuwa wote
waheshiwa wabunge tunamuunga mkono Rais wetu katika uchumi wetu.”
Manyanya ameyasema hayo leo Mei 11, 2018 wakati akijibu hoja
mbalimbali za wabunge walizozitoa wakati wakijadili hotuba ya bajeti ya wizara
hiyo ya mwaka 2018/19 ya Sh143.3 bilioni
Kadhalika, Manyanya amesema tafsiri ya viwanda ni eneo
ambalo shughuli ya kiuchumi hufanyika kwa lengo la kuzalisha bidhaa
“Tumeandaa kitabu chenye orodha ya viwanda vyote na viwanda
ni sawa na binadamu, wanazaliwa, wanakuwa na wanakufa hivyo hivyo kwa viwanda,”
amesema
Kuhusu ulipaji wa fidia kwenye maeneo ya uwekezaji, Manyanya
amesema tayari kuna fedha zimetengwa za kulipa fidia akitolea mfano Ruvuma Sh2
bilioni zimetengwa
Manyanya akizungumzia Tume ya Ushindani (FCC), amesema
Serikali inaendelea kushirikiana na wazalishaji mbalimbali ili kupata utambuzi
mzuri wa bidhaa na kuondoa usumbufu uliopo kwa kutumia teknolojia ya habari na
mawasiliano
Amesema suala la kuuza ufuta kwa kutumia stakabadhi gharani
mchakato unafanyika ikiwamo kufanyika kwa kikao cha wadau hivi karibuni jijini
Dodoma
Waziri Manyanya apangua hoja za wabunge
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 11, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 11, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment