Wanausalama wa viwanja
mbalimbali vya ndege nchini, wameiva na kuimarika katika usalama wa vifurushi
na mizigo inayosafirishwa kwa njia ya ndege baada ya kufuzu mafunzo
yaliyoendeshwa na wakufunzi kutoka Taasisi ya Kimataifa ya Usafiri wa Anga
(ICAO).
Wakati akifunga mafunzo hayo Kaimu
Mkuu wa Kitengo cha Viwango cha Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania, Bw.
Vedastus Fabian kwa niaba ya Kaimu Mkurugenzi Mkuu, amewataka wahitimu hao
kutumia vyema ujuzi walioupata kwa kufanyakazi kwa ufanisi na kuboresha kazi
hiyo, ili kuepuka kupitisha mizigo hatarishi kwa usalama wa usafiri wa anga.
“Tunavyojua mfumo wa usafiri wa anga
duniani ni moja kwa hiyo tunavyoonesha usalama katika viwanja vyetu vya ndege
hapa Tanzania kunajenga imani kubwa kwa mashirika ya ndege na wadau wote
wanaofanya shughuli nakutumia viwanja vyetu vya ndege, hivyo tutaongeza wingi
wa mizigo,” amesema Bw. Fabian.
Aidha ametoa pongezi kwa wahitimu
hao 19 walio Chuo cha Usafiri wa Anga kilichopo katika Jengo la
Kwanza la Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA-TBI) na
kuweza kufaulu vyema mafunzo hayo, ambapo sasa watakuwa na weledi na ufanisi
bora katika kazi hiyo.
Amesema TAA inategemea mafunzo hayo
yataleta manufaa na sio kuonesha vyeti ukutani kuwa wamehitimu bali ni kuonesha
ujuzi walioupata kutasaidia kutambua mizigo na vifurushi vyenye matatizo ya
kutishia usalama wa anga na kuongeza uhakika wa safari za anga.
Bw. Fabian pia amesema wanategemea
washiriki kufikisha na kusambaza ujuzi huo kwa wanausalama wengine, ambao
hawakupata fursa ya kushiriki mafunzo hayo adimu, ili nao waboresha kazi zao.
Wanausalama wa Viwanja vya ndege waimarika
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 19, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 19, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment