Wabunge wameitaka Serikali kuchukua hatua ikiwamo kuwataka
wanasiasa walioonekana wakiwachoma sindano ya kuzuia saratani ya mlango wa
kizazi, kuomba radhi na kuwalipa fidia watoto hao
Hata hivyo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee
na Watoto, Ummy Mwalimu amesema kilichofanyika ni majaribo huku akikiri kushika
sindano kama si mtaalamu ni makosa
Hayo yamejitokeza leo Mei 3, 2018 bungeni mjini Dodoma
wakati wabunge wakiomba mwongozo wa Spika, wakitumia kanuni ya 67 (8) ya jambo
lililotokea hivi karibuni
Aliyeanzisha alikuwa mbunge wa Viti Maalum (Chadema),
Anatropia Theonest aliyehoji kuwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii,
wamejitokeza madaktari wa ghafla wakiwamo wakuu wa wilaya na wabunge,
wakichanja watoto
“Sasa nimepata taharuki, sisi kama hatuna taaluma,
tunachomaje sindano, nimesikia waziri ametoa kauli lakini haitoshi, nimesoma
miiko ya madaktari hairuhusu, nimesoma miiko ya wauguzi hakuna,” amesema
Katika kusisitiza hilo, Theonest amesema; “Madaktari
wamevunja miiko, wauguzi wamevunja miiko na wanasiasa hao wamevunja maadili
yao. Naomba hao watu waliochoma sindano wawaombe radhi na watoto wapewe fidia
na mabaraza husika yanachukua hatua gani katika hilo?”
Mbunge mwingine wa Viti Maalum (Chadema), Anna Gidarya alimuunga
mkono Theonest akisema; “Huwezi kwenda tu kumchoma, chanjo ndizo zinaleta
matatizo hata sisi wataalamu tunajua.”
Akitoa majibu ya miongozo hiyo, Spika Job Ndugai amesema,
“Tunawaachia Serikali walifuatilie.”
Waziri Mwalimu alijibu miongozo hiyo akisema
“Nakiri, uchomaji wa sindano una taratibu zake, huwezi
kujichomea ovyo ovyo, nawahakikishia Mshana na Mlinga hawakuwachoma chanjo
watoto husika ila walifanya kama majaribio.”
Mwalimu amesema ametoa maagizo kwa waganga wa mkoa na wilaya
na kuwaeleza kuwa hata kushika sindano ni makosa
Wakuu wa Wilaya, wabunge waliowachoma sindano mabinti watakiwa kuomba radhi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 03, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 03, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment