Viongozi wa dini wameaswa kuepuka
migogoro ya mara kwa mara katika makanisa yao na badala yake waendelee
kuwajenga waumini wao wakue kiroho na kujenga dhana ya umoja na upendo katika
Taifa
Pia imesema inawashukuru viongozi wa
dini na madhehebu yote ya dini kwa kuendelea kuiombea nchi amani, mshikamano na
utulivu, jambo ambalo linaongeza chachu kubwa kufikia mafanikio ya maendeleo ya
kijamii, kisiasa na kiuchumi
Hayo yamesemwa leo na Waziri Mkuu
Kassim Majaliwa katika ibada ya kutawazwa Askofu Dkt. Maimbo Mndolwa wa
Dayosisi ya Tanga kuwa Askofu Mkuu wa saba wa Kanisa la Anglikana Tanzania.
Ibada hiyo imefanyika katika Kanisa
Kuu la Roho Mtakatifu Dayosisi ya Central Tanganyika Jijini Dodoma
“Nawaombeni wote kwa ujumla wetu,
tuendelee kutumia makanisa yetu kuombea Taifa hili ili tuendelee kuishi kwa
amani, upendo na mshikamano. Watu wa Mungu ni watu wa upendo, watu wa
Mungu ni watu wa amani, watu wa Mungu ni watu wa kiroho,” amesema
Waziri Mkuu ameongeza kuwa:
“Haitarajiwi kuona watu wa Mungu wakiwa katika mstari wa mbele kuchochea
migogoro, kuvunja amani ya kanisa na kuongoza makundi yanayopingana katika kazi
ya Bwana.”
Viongozi wa dini waaswa kuepuka migogoro
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 20, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 20, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment