TRA yatishia kuuza mali za Makonda

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) inakusudia kufanya mnada wa wazi mwezi ujao kwa mizigo iliyokaa bandarini kwa muda mrefu bila kukombolewa, ikiwamo ya Paul Makonda

Hata hivyo, ofisa wa TRA aliyetafutwa jana, hakutaka kueleza kama jina la Makonda lililopo katika tangazo hilo ni la mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, na kiongozi huyo wa mkoa alipotafutwa, hakupatikana kuzungumzia suala hilo

Haikuweza kufahamika kama shehena hiyo imetolewa katika muda wa siku tano tangu tangazo hilo litoke kutokana na TRA kutotaka kuzungumzia suala hilo kwa kina na kutopatikana kwa wamiliki

Kwa mujibu wa tangazo lililotolewa Mei 12 na Kaimu Kamishna wa Forodha na Ushuru wa TRA, Ben Asubisye na kuchapishwa katika gazeti la Serikali, Daily News, wamiliki wanatakiwa kuitoa mizigo hiyo ndani ya siku 30 kuanzia siku ilipotangazwa

Katika tangazo hilo lenye orodha ya makontena zaidi ya 800, jina la Paul Makonda limejitokeza mara 20 akiwa mpokeaji wa makontena 20 yaliyopo katika bandari kavu ya DICD yakiwa na bidhaa kadhaa, kama samani

Ingawa hakuna uthibitisho kuwa Makonda ndiye mwenye makontena hayo, Februari 16 mkuu huyo wa mkoa alikaririwa katika mtandao wa gazeti la Serikali la HabariLeo kuwa alipokea makontena 20 yenye samani zitakazotumika katika ofisi za walimu zinazoendelea kujengwa. Mzigo huo ulikuwa sehemu ya shehena ya makontena 36

Samani hizo za ofisini zilizokuwa na thamani ya Sh2 bilioni, zilitolewa na Watanzania wanaoishi Marekani wanaojulikana kama Six Region Diaspora Council

Juhudi za kumpata Makonda ili kuzungumzia suala hilo zilishindikana na hata alipotumiwa ujumbe mfupi wa maneno (sms) hakujibu

Alipotafutwa na Mwananchi, mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi wa TRA, Richard Kayombo alisema mamlaka imetoa notisi ya siku 30 kwa waagizaji wa mizigo ambao mizigo yao imekaa bandarini kwa zaidi ya siku 90

“Tangazo lililotolewa ni notice (taarifa) kwa wahusika ili wakomboe mizigo yao ndani ya siku 30. Isipokombolewa itanadiwa. Mizigo hiyo inaweza kuwa ni ile ambayo haijalipiwa kodi au hata ile iliyolipiwa lakini haijaondolewa,” alisema

Alipoulizwa kama shehena hiyo ni mali binafsi ya Makonda au ya ofisi yake, Kayombo alisema: “Majina yaliyoandikwa kwenye magazeti ndiyo taarifa za consignees (wapokeaji) zilizo kwenye nyaraka. Madhumuni ya matumizi siyo sehemu ya wajibu wetu


TRA yatishia kuuza mali za Makonda TRA yatishia kuuza mali za Makonda Reviewed by KUSAGANEWS on May 17, 2018 Rating: 5

No comments: