Serikali yafuta leseni zote za kuhodhi maeneo ya madini


Serikali imefuta leseni zote za kuhodhi maeneo ya madini na wamiliki wake wametakiwa kuomba upya wakizingatia Sheria ya Madini na kanuni zake.

 Akizungumza na waandishi wa habari leo Ijumaa Mei 11, 2018  Mwenyekiti wa Tume ya Madini nchini, Profesa Idris Kikula amesema tangazo la Serikali namba moja la mwaka 2018 limesema maeneo yote yaliyopewa leseni yanarejeshwa serikalini bila hakikisho la kupewa tena

Amesema uamuzi huo umefanyika kwa mujibu wa Sheria ya Madini ya mwaka 2019 ikisomwa na marekebisho yake ya mwaka 2017 na kanuni ya 21 ya kanuni za Madini (Haki Madini za mwaka huu).
Amesema leseni zilizofutwa na wamiliki wake wanatakiwa kuomba tena zinazihusu kampuni 11, kwamba leseni hizo zinajumuisha migodi ya kati na mikubwa

Migodi hiyo ni pamoja na Kabanga Nickel Company Limited, National,Mineral Development Corporation Limited, Bafex Tanzania Limited ambayo inamiliki leseni za maeneo matatu

Nyingine ni Mabangu Mining Limited, Resolute (Tanzania) Limited,  Wigu Hill Mining Company Limited, Nachingwea Nickel Limited na Precious Metals Refinery Company Limited.
Serikali yafuta leseni zote za kuhodhi maeneo ya madini Serikali yafuta leseni zote za kuhodhi maeneo ya madini Reviewed by KUSAGANEWS on May 11, 2018 Rating: 5

No comments: