Kamanda wa
Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Lazaro Mambosasa amempongeza Mtanzania
anayeishi Marekani, Mange Kimambi kwa maelezo kuwa ameipongeza Serikali
Mambosasa
ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Mei 11, 2018 katika mkutano wake wa waandishi wa
habari na kumpongeza Mange ambaye alikuwa kinara wa kushawishi watu kuandamana
Aprili 26, 2018 katika maadhimisho ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar
Kamanda huyo
amesema Watanzania wanatakiwa kufika mahali wachague watu wa kuwashabikia
"Aprili
26 wananchi wa kanda yangu walipuuza uhamasishaji wake katika mitandao ya
kijamii, sasa Mange huyo huyo anaipongeza Serikali,” amesema
Amesema kwa
kuwa ameipongeza Serikali nao wanampongeza kwa kuwa sasa amerudi kundini
"Nampongeza
kwa kuwa amerudi kundini alikuwa anapotosha na Watanzania walipopuuza na yeye
ameamua kurudi na kuipongeza Serikali,” amesema Mambosasa
Kuhusu
watuhumiwa waliokamatwa wakihusishwa na maandamano ya Aprili 26, Mambosasa
amesema walioshukiwa kufanya walihojiwa na kupata dhamana.
Mambosasa ampongeza Mange Kimambi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 11, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 11, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment