RAISI MAGUFULI TUSAIDIE WANANCHI WA KIJIJI CHA KINKO KATA YA LUKOZI TUMEUZIWA MAENEO YA SERIKALI ZAIDI YA EKARI 40

Wananchi wa kijiji cha Kinko kata ya Lukozi wilayani Lushoto mkoani Tanga wameiomba serikali ya awamu ya Tano kuwasaidia kurejeshewa maeneo ya mashamba ya serikali yaliouzwa kwa matajiri wachache kwenye eneo hilo likiwemo eneo lililoko nyuma ya ofisi ya Chama cha mapinduzi.

Akizungumza mmoja wa mzee ambaye ni mzawa wa eneo hilo ambaye alitaka jina lisitajwe amesema kuwa kuanzia miaka ya 1960 maeneo hayo makubwa ambayo yalikuwa ni mali ya Serikali yaliuzwa kimya kimya bila wao kujua walishangaa watu wanayalima bila taarifa kutoka kwa viongozi.

Amesema kuwa aliyehusika kuuza maeneo hayo ni mwenyekiti aliyemaliza muda wake ambaye ni Bwana Shabani Mweri ambaye aliuza mashamba ya kijiji ,na maeneo yote ya maji (vitivo)ambapo kwasasa kijiji hicho kimebakia na maeneo machache tu.

Ameongeza kuwa eneo la mashamba ya kijiji yalikuwa zaidi ya Ekari 40 lakini mpaka kufikia sasa kuna ekari ambazo hata hazizidi 22 baada ya maeneo mengine kuuzwa.

“Kipindi hicho maeneo kweli yalikuwa makubwa lakini bwana mweri akawauzia matajiri tajiri wa hapa kijijini kina mzee Saidi Mdoe,Kina Ibrahimu ,na watu wengine kutoka nje ya hapa sasa tunauliza mwenyekiti anapata mamlaka wapi ya kuuza maeneo?”Alisema mzee huyo

Hata hivyo amesema wanamtaka mkuu wa wilaya ya Lushoto Mh Januari Lugangika kwa kuwa ndiye muakilishi wa raisi afike katika kijiji hicho na wako tayari kuonyesha maeneo yaliouzwa na mwenyekiti aliyemaliza muda wake bwana Shabani Mweri 

Naye mmoja wa mwananchi katika eneo hilo amesema kuwa baadhi ya watu walijaribu kufuatilia na kuhoji kuhusu maeneo yaliouzwa lakini walibaki kutishiwa maisha na wengine kuishia polisi kwa kesi za kusingiziwa.

“Kweli bwana watu walijitokeza kupiga kelele lakiniwalishia kuonekana wao ndiyo wabaya akiwemo mtendaji ambaye yupo kwasasa amepambana mpaka wamepelekana mahakamani lakini matajiri wakatoa rushwa na kupewa maeneo ambayo kwasasa wanayamiliki na sisi kama wananchi tunaogopa”Alisema

“Tunajua Raisi huku hawez kufika mana ana majukumu mengi lakini anawasaidizi wake kama mkuu wa wilaya aje atusimamie tupate haki yetu tuliodhulumiwa na watu wachache jamani kwanini lakini , tunataka maeneo yetu tunamuamini raisi magufuli”Aliongeza

Hata hivyo tulizungumza na aliyekuwa mwenyekiti wa kijiji hicho Bwana Charles Mavoa na kukiri ni kweli maeneo mengi yameuzwa lakini kwa nfasi yake alipambana lakini hakuweza kwasababu hakupata uungaji mkono wowote.

Naye mwenyekiti wa sasa katika kijiji hicho bwana Kirua Mhina amesema bado kwa nafasi yake wanashirikiana kujua ni namna gani ya kurudisha maeneo hayo yaliouzwa na watu wachache kwa maslahi yao binafsi.

Pamoja na hayo tulizungumza na mkuu wa wilaya ya Lushoto Bwana Januari kuhusu malalamiko hayo nakusema kuwa anapanga ziara rasmi katika maeneo hayo ili waone ni jinsi gani ya kupata ukweli wa malalamiko hayo ya wananchi.

Juhudi za kumtafuta mwenyekiti aliyehusika kuuza maeneo hayo Bwana Shabani Mweri zinaendelea na kupitia muandishi wako endelea kufuatilia zaidi Kusaganews

RAISI MAGUFULI TUSAIDIE WANANCHI WA KIJIJI CHA KINKO KATA YA LUKOZI TUMEUZIWA MAENEO YA SERIKALI ZAIDI YA EKARI 40 RAISI MAGUFULI TUSAIDIE WANANCHI WA KIJIJI CHA KINKO KATA YA LUKOZI TUMEUZIWA MAENEO YA SERIKALI ZAIDI YA EKARI 40 Reviewed by KUSAGANEWS on May 11, 2018 Rating: 5

No comments: