Mbunge CUF adai Serikali ‘inabeti’, azua hekaheka bungeni


Kauli ya  mbunge wa Tandahimba (CUF), Katani Katani ya kufananisha utendaji kazi wa Wizara ya Kilimo na michezo ya kubahatisha maarufu kama ‘kubeti’ imezua kisaazaa bungeni

Kauli hiyo aliyoitoa leo Mei 15, 2015 katika mjadala wa bajeti ya wizara hiyo mwaka 2018/19 ulimuinua kwenye kiti  Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Jenista 

Mhagama na kusema kauli ya Katani inawadhalilisha walioko serikalini

Katika maelezo yake Katani amesema hadi leo mawakala wanaosambaza pembejeo hawajalipwa fedha zao.

 Amesema Sh200bilioni  zilizotakiwa kwenda katika mfuko wa korosho hazijaenda kwa miaka yote kwa ajili ya kukuza zao

“Serikali hii imekuwa ya kubeti beti na kwenye  kilimo imekuwa ikibeti. Fedha za korosho za export levy (ushuru wa mazao yanaouzwa nje) Sh206bilioni hazilipi. Mnacheza na  kilimo, mnawadanganya wakulima wa korosho,”amesema

Amesema Waziri wa Kilimo, Dk Charles Tizeba amekuwa akikibeba chama cha ushirika cha Tanecu kwa kukiombea kukopeshwa fedha Sh 200bilioni

Amehoji pia sababu ya msingi ya kumuondoa mkurugenzi wa bodi ya korosho na kuwaacha watendaji.

 “Kwanini wasingeondolewa watendaji? Hakuna maelezo yanayotosheleza yaliyosababisha mkurugenzi huyu kuondolewa,”amesema

Hata hivyo, Katani aliombewa utaratibu na Mhagama kuwa lugha anayoitumia inadhalilisha watu wanaofanya kazi Serikalini kwasababu neno kubeti lina maana ya kubahatisha

Hatua hiyo ilimfanya Mwenyekiti wa Bunge Andrew Chenge kumtaka kufuta maneno hayo lakini Katani akaendelea kufafanua alichokuwa akikikimaanisha na hivyo kutakiwa na kiti kutoendelea kuchangia

Mbunge CUF adai Serikali ‘inabeti’, azua hekaheka bungeni Mbunge CUF adai Serikali ‘inabeti’, azua hekaheka bungeni Reviewed by KUSAGANEWS on May 15, 2018 Rating: 5

No comments: