Rais John Magufuli ameiomba Serikali ya Denmark kusaidia
ujenzi wa kipande cha barabara ya kilomita 11 katika Mkoa wa Iringa ili
kuwezesha malori kutopita katikati ya mji huo na kupunguza ajali zinazotokea
Rais Magufuli amesema hayo leo Mei 3 wakati akizindua
barabara ya Iyovi – Iringa – Mafinga yenye urefu wa kilomita 218 iliyojengwa
kwa mkopo nafuu kutoka serikali ya Denmark na kugharimu Sh283 bilioni
Amesema mpango huo ulikuwepo tangu alipokuwa wizara ya
ujenzi na kufafanua kwamba malori yanayopita katikati ya mji wa Iringa yamekuwa
yakisababisha ajali kwa wakati wa mji wa huo
“Nakuomba Balozi, hili mlichukue kama la urgent (haraka),
mkitusaidia kama mkopo sisi tuko tayari, mkitupa kama grant (msaada)
tutashukuru zaidi. Kwa hiyo tunaomba utufikishie hili, ikiwezekana barabara
hiyo tutaiita Pamela Road,” amesema Rais Magufuli huku wananchi wakipiga makofi
Rais Magufuli amewataka wananchi wa Iringa kuitumia barabara
ya Iyovi – Iringa – Mafinga kama fursa ya kujiongezea kipato na kukuza uchumi
wao. Amesema barabara hiyo ni kiungo muhimu kwa shughuli za kiuchumi
Amesema miundombinu ya barabara ni muhimu pia kwa uchumi wa
viwanda kwa sababu inarahisisha bidhaa zinazotengenezwa viwandani kusafirishwa
kwa urahisi kwenda kwenye masoko mbalimbali nchini au nje ya nchi
Awali, Rais Magufuli alizindua kiwanda cha kutengeneza
chakula cha kuku cha Silverland Tanzania Ltd mkoani humo na kuwapongeza
viongozi wa mkoa huo kwa kuvutia uwekezaji wa viwanda na amepewa taarifa kwamba
mpaka sasa mkoa huo una viwanda 2,963
“Kukamilika kwa barabara hii kutafungua fursa nyingi, sasa
wananchi mtaweza kusafirisha mazao yenu kuleta kwenye kiwanda cha Silverland,
nao wataweza kusafirisha chakula cha kuku kwenda sehemu mbalimbali. Ni jukumu
letu kuwajengea mazingira wezeshi kibiashara,” amesema
Magufuli aiomba Denmark kusaidia ujenzi wa barabara
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 03, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 03, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment