Kamanda Mwaibambe afunguka kususiwa maiti


Kamanda wa Polisi mkoa wa Kipolisi Tarime/Rolya Henry Mwaibambe, amesema kwamba tuhuma zinazoenea mitandaoni kuhusu tofauti iliyopo kati ya jeshi la Polisi na familia ya marehemu Suguta aliyeuawa na polisi hadi kufikia kutaka kususa kuzika maiti, sio za kweli kwani wana ushirikiano mzuri.

Akizungumza  Kamanda Mwaibambe amesema kama jeshi la polisi wametoa ushirikiano wao tangu tukio la mauaji lilipotokea kwa kutoa taarifa kwa familia, kuelezea mazingira ya tukio, na kuwashirikisha hata kwenye 'postmoterm', na hata baada ya kikao cha familia kupita, walishirikishwa.

"Hakuna mgogoro wowote, hakuna fujo ya aina yoyote watu wametulia wanaendelea na shughuli zao, tuliwaambia ukweli tukio limetokea, tukazungumza na wanafamilia, hata 'postmoterm' tuliwaambia, na hata wao walipokaa kikao cha familia wakaamua kwamba tutauzika mwili wa ndugu yetu kwa heshima zote na kila kitu tunashirikiana nao”, amesema Kamanda Mwabambe

Sambamba na hilo Kamanda Mwaibambe amesema alifuatilia kwa kina kujua nini chanzo cha skari huyo kumuua Chacha Suguta, na kubaini ni mgogoro uiojitokeza baada ya kumwambia maneno yasiyofaa.

"Nimefuatilia kuna maneno ambayo ya kilugha yalitamkwa kwa Kikurya ingawa siwezi kuyasema moja kwa moja, ndio yalimsababisha yule askari apate jazba namna hii, ila yalikuwa maneno yasiyofaa ”, amesema Kamanda Mwaibambe.

Chacha Suguta ambaye ni mdogo wa Mbunge wa Tarime vijijini John Heche aliuawa kwa kuchomwa kisu na polsi aliyemkamata, April 27, 2018.

Kamanda Mwaibambe afunguka kususiwa maiti Kamanda Mwaibambe afunguka kususiwa maiti   Reviewed by KUSAGANEWS on May 02, 2018 Rating: 5

No comments: