Sakata la
mradi wa umeme wa Stigler’s Gorge ambao utekelezaji wake unafanyika katika pori
la akiba la Hifadhi ya Selous, limeibuka tena bungeni leo jioni Mei 22, 2018 na
kuzua mvutano huku Spika Job Ndugai akieleza kutoridhishwa na majibu ya
Waziri wa Maliasili na Utalii
Suala hilo
lilitikisa Bunge leo mchana baada ya wabunge kadhaa kuhoji utekelezaji wa mradi
huo, kueleza athari za kimazingira zinazoweka kujitokeza
Selous ni
miongoni mwa mapori yanayotambuliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu na
Utamaduni (Unesco) kama sehemu ya urithi wa dunia, lakini uamuzi wa Serikali
kuzalisha zaidi ya megawati 2,100 ikitumia zaidi ya Dola 2bilioni (zaidi ya
Sh4.5trilioni) unaelezwa kuwa huenda ukaliondoa pori hilo kwenye orodha hiyo
Bunge
lilipokaa kama kamati leo jioni kupitisha bajeti ya Wizara ya Maliasili na
Utalii mwaka 2018/19 ya Sh115bilioni, mbunge wa Ulanga (CCM), Godluck Mlinga
alianza kwa alihoji kama Serikali itakuwa na mkakati mzuri wa kuwasaidia
wananchi wanaoishi katika maeneo hayo
Hoja ya Mlinga
iliungwa mkono na Ndugai aliyeitaka Wizara ya Nishati kuwa makini na
kutengeneza utaratibu wa kupanda miti katika maeneo mbalimbali yanayoanzishwa
miradi ya umeme
Ndugai amesema
katika maeneo mengi Wizara hiyo imekuwa na utaratibu wa kukata miti mingi
katika utekelezaji wa miradi lakini inakosa usimamizi wa upandaji miti mingine
“Mheshimiwa
Mlinga naamini kuwa wamekuelewa lakini na ninyi Nishati lazima muwe na
mipango mizuri ya kupanda miti katika miradi yenu. Haiwezekani unakata miti
lukuki lakini hakuna mpango wa kuipanda hiyo haikubariki kabisa,” amesema
Ndugai
Ndugai ambaye
pia aliungwa mkono na mbunge wa Kigoma Mjini (ACT-Wazalendo), Zitto Kabwe kwa
pamoja walipingana na majibu ya Waziri wa Nishati, Dk Medard Kalemani kuhusu
upandaji wa miti katika eneo hilo
Wakati wawili
hao wakitaka kusikia majibu ya Serikali kuhusu utunzaji wa mazingira katika
eneo hilo, ikiwa ni sambamba na kupanda miti baada ya kuikata iliyopo, Dk
Kalemani hakuwa akitoa majibu ya kina kuhusu hoja yao hiyo
Katika majibu
yake Dk Kalemani amesema miradi inayoanzishwa itakuwa na mipango mizuri hata ya
uhifadhi wa mazingira, huku akijikita zaidi kueleza mpango wa kuongeza nguvu ya
uzalishaji umeme nchini
“Yaani Waziri
hujatuelewa kabisa tunachotaka sisi ni hii miti mingi mnayokata halafu
mnakusanya na hampandi mingine, hivi hamjui habari ya uhifadhi kweli basi
nimemaliza, nimemaliza waziri usisimame tena,” amesema Ndugai baada ya waziri
huyo kuomba kujibu tena huku wabunge wakipiga
Naibu Waziri
Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira), Kangi Lugola amesema mradi huo
hauna madhara kwa wananchi na Taifa kwa ujumla, akijitokeza mtu akaupinga
atafungwa bila huruma.
Bajeti Maliasili na Utalii yapita, mradi wa Stigle’s Gorge watikisa
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 22, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 22, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment