Watu watatu
wamefariki dunia na wengine wawili kujeruhiwa baada ya gari walilokuwa wakisafiria
kuelekea Dodoma kupinduka.
Ajali hiyo
imetokea jana jioni Jumatatu Mei 21, 2018 eneo la Mtelela Barabara ya Msolwa
Chalinze mkoani Pwani
Akizungumza mganga
wa zamu wa kituo cha afya Msoga, Dk Nelson Luoga amesema wamepokea majeruhi
wawili; Priscus Chuwa na Godfrey Kilolo ambao wote ni watumishi wa kituo
cha uwekezaji (TIC).
Amesema
waliwapa huduma ya kwanza lakini baada ya hali zao kubadilika waliwapa rufaa
kwenda Hospitali ya Tumbi Kibaha na baada ya vipimo zaidi usiku wa kuamkia leo
walipelekwa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH
Amesema
waliofariki ni watumishi wa umma, kubainisha kuwa katika kituo hicho
hawakupokea miili ya watu hao, zaidi ya majeruhi ambao tayari wamehamishiwa
Muhimbili.
Ajali yaua watatu, yajeruhi wawili
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 22, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
May 22, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment