Wakati Mzazi
mwenzie akiendelea kukabaliana na misukosuko mbalimbali, Zarina Hassan ametua
kwa mara ya pili nchini kimyakimya
Zari ametua leo mchana akitokea
nchini Afrika Kusini yalipo makazi yake akisema amekuja kupiga picha za
bidhaa za nepi za watoto aina ya SoftCare, zinazotengenezwa na kiwanda cha
Kedz Tanzania
Mama huyo wa watoto watano na
mjasiriamali maarufu, alitangazwa rasmi kuwa balozi kwa miaka mitatu wa
bidhaa hizo Machi 28 mwaka huu
Meneja masoko wa Kedz, Briton
Mkocha ambaye ndiye alifika kumpokea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa
Julius Nyerere (JNIA), aliiambia Mwananchi kuwa moja ya shughuli zilizomleta
kufanya Zari ni pamoja na kupiga picha za video zitakazotumika kwa tangazo la
bidhaa hiyo
Kwa upande wake Zari amesema
anajisikia furaha kufanya kazi kampuni hiyo na kueleza kuwa kuna wanawake
wengi na warembo hapa Tanzania huenda wangeamua kufanya nao kazi, lakini
wameamua kumchagua yeye jambo ambalo ni heshima kwake
|
Zari atua nchini kimyakimya
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 19, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment