ZAIDI YA WTOTO 20,000 ARUSHA KUPATIWA CHANJO YA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI


Zaidi ya watoto elfu ishirini wenye umri wa miaka 14 kutoka wilaya zote saba za Mkoa wa Arusha wanatarajiwa kupatiwa chanjo ya saratani ya shingo ya kizazi ili kuwakinga na ugonjwa huo

Mratibu wa Chanjo Mkoa wa Arusha Aziz Sheshe amesema chanjo hiyo itaanza kutolewa rasmi tarehe 25 mwezi huu katika vituo vya afya 292 na katika shule zitakazo ainishwa ikiwa ni pamoja na vituo maalum vitakavyokuwa katika ofisi za vijiji.

Katibu tawala wa Mkoa wa Arusha  Richard Kwitega  amesema ni vema jamii ikaondokana na mila potofu  na  upotoshaji  utakaokwamisha zoezi hilo kwani chanjo hiyo ni salama  na itaokoa maisha ya watoto wa kike; kwa kuwa hadi sasa asilimia 50 ya vifo vyote vinatokana na saratani ya shingo ya kizazi na matiti.

Naye mganga Mkuu wa Mkoa wa Arusha Timothy Onanji ameeleza kuwa  chanjo hiyo ni juhudi za serikali ili kuleta maendeleo katika kupambana na ugonjwa huo unaokua kwa kasi. 

Aidha Naibu meya wa Jiji la Arusha Viola Lazaro akiongea kwa niaba ya wanawake amesema  chanjo hiyo ni mkombozi kwa wanawake  katika taifa kutokana na matibabu ya ugonjwa huo kuwa na garama kubwa hivyo wajitokeze kwenda kupata chanjo hiyo kwani afya njema inajenga taifa  bora.

ZAIDI YA WTOTO 20,000 ARUSHA KUPATIWA CHANJO YA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI ZAIDI YA WTOTO 20,000 ARUSHA KUPATIWA CHANJO YA SARATANI YA SHINGO YA KIZAZI Reviewed by KUSAGANEWS on April 17, 2018 Rating: 5

No comments: