Baadhi ya
maeneo yamefunikwa na maji Kenya kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha nchini
humo huku zaidi ya watu 228,000 wakihitaji msaada maalumu ikiwamo chakula na
dawa.
Mvua hizo zimesababisha vifo,
maporomoko ya ardhi na uharibifu wa miundombinu kwa kiasi kikubwa pembe nyingi
za nchi hiyo yamesababisha idadi kubwa ya wananchi kukosa mahali pa kuishi
baada ya nyumba zao kubomoka.
Katika
kaunti ya Tana River, Gavana Dhadho Godhana alisema asilimia 70 ya wakazi
wameathiriwa huku watu 11 wakidaiwa kupoteza maisha kwa kusombwa na
mafuriko.
Akizungumza na waandishi wa
habari mjini Nairobi, Gavana Dhadho alisema miongoni mwa waliopoteza maisha ni
pamoja na watoto wadogo.
Gavana huyo
alisema mbali na Mto Tana kuvunja kingo zake, mito mingine midogo inayoanzia
kaunti za Kitui na Makueni imejaa maji na kusababisha uharibifu mkubwa wa mali
na watu kupoteza maisha.
“Katika
baadhi ya maeneo watu wanaishi katika kambi 106. Familia 38,000 zimeathiriwa
moja kwa moja na mafuriko,” aliongeza Gavana Dhadho.
Alisema
watu 228,000 wanakabiliwa na hatari ya kupata maradhi, hawana makazi, chakula,
dawa, maji safi na mahitaji mengine.
“Watu
wanaoishi kando ya Mto Tana wanakabiliwa na tisho kuu la njaa baada mimea yao
kuharibiwa na mafuriko,” alisema.
Hali
ya uchukuzi pia imeathiriwa na misaada inaweza kupelekwa kwa ndege au kwa
mashua.
Gavana Dhadho alitoa wito kwa
mashirika ya kutoa misaada kujitokeza kuungana na Serikali yake kusaidia
waathiriwa.
Kamishna wa kaunti hiyo
Michael Kioni alisema kaunti ndogo ya Tana Kaskazini ndiyo imeathirika sana,
familia 16,000 zimeathirika ikifuatiwa na ile ya Tana Delta ambapo familia
14,000 zimeathirika. Kaunti ndogo ya Tana River ni ya tatu ambayo ina
waathiriwa 8,000.
Wakati huohuo watu
nane walikufa baada ya kusombwa na mafuriko katika matukio tofauti Kaunti
ya Kisii kufuatia mvua hiyo inayoendelea kunyesha kote nchini.
Mtu
mmoja alisombwa na maji katika eneo la Nyambunde, Kaunti ndogo ya Bobasi
alipokuwa akivuka daraja kwenye Mto Gucha uliofurika.
Katika
eneo la Ogembo, watu wawili walipoteza maisha baada ya kusombwa na maji
walipokuwa wakijaribu kuvuka mto huo.
Mvua
hiyo ilisababisha uharibifu mkubwa kwenye mashamba huku nyumba zilizokuwa
karibu na mto huo zikiharibiwa pia.
Eneo
la Daraja Mbili, mjini Kisii watu wengine walikufa maji baada ya kujaribu
kuvuka daraja na kusombwa na Mto Nyakomisaro.
Watu
zaidi ya 100 kutoka maeneo ya Mugirango Kusini na Bobasi, hawana makazi baada
ya nyumba zao kusombwa na mafuriko.
Msimamizi
wa Idara ya Majanga katika Kaunti ya Kisii Dk Walter Okib alisema kuwa mvua
hiyo imesababisha hasara katika maeneo hayo na kusababisha vifo kadhaa.<
Watu 228,000 wahitaji dawa, chakula Kenya
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 30, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 30, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment