Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amesema
bajeti ya wizara hiyo mwaka 2018/19 imepungua kwa asilimia 19.6 ikilinganishwa
na ya 2017/18 kutokana na dhamira ya Serikali kutumia fedha za ndani
kuitekeleza
Akijibu hoja zilizoibuka wakati wa
mjadala wa hotuba ya bajeti ya wizara hiyo, Ummy alisema mwaka jana wabunge
waliishauri Serikali kupunguza utegemezi kutoka wa wafadhili katika kutekeleza
bajeti ya afya
Bajeti ya wizara hiyo mwaka 2018/19
ni Sh898.3 bilioni tofauti na mwaka 2017/18 unaoishia Juni ya Sh1.07 trilioni
“Waheshimiwa wabunge, mwaka jana
wakati nawasilisha bajeti hapa mlieleza wazi kwamba bajeti inategemea
wafadhili. Kilichotokea bajeti Wizara ya Afya kwa mwaka huu fedha za ndani
zimeongezeka kutoka Sh628 bilioni hadi Sh681 bilioni lakini fedha kutoka kwa
wafadhili zimeshuka,” alisema Ummy
“Hii imeonyesha dhamira ya Rais John
Magufuli kutaka kupunguza utegemezi wa wadau wa maendeleo katika kupunguza
changamoto za Watanzania.”
Alisema lengo ni nchi kuanza
kujipima yenyewe katika utekelezaji wa bajeti ili kuona ni kwa namna gani
inaweza kutatua changamoto zilizopo
Juzi, Kamati ya Bunge ya Huduma za
Jamii ilieleza kuwa bajeti ya wizara hiyo imepungua kwa asilimia 19.6 na kwamba
kutaleta athari katika utoaji wa huduma kwa wananchi
Mwenyekiti wa kamati hiyo, Peter
Serukamba alisema katika bajeti ya mwaka 2017/18, fungu la fedha za maendeleo,
wizara ilitengewa Sh785 bilioni na hadi kufikia Februari Sh385.77 bilioni,
kiasi ambacho ni sawa na asilimia 49 kilipokewa na ili kutekeleza miradi
Alibainisha kuwa kati ya fedha hizo
za maendeleo, Sh336.3 bilioni ni za kutoka vyanzo vya ndani na Sh449.5 bilioni
kutoka vyanzo vya nje
“Kamati imebaini fedha zilizopokewa
kutoka vyanzo vya ndani ni Sh64.7 bilioni sawa na asilimia 19 ya fedha
zilizoidhinishwa. Fedha za nje zilizopokewa ni Sh321 bilioni sawa na asilimia
71,” alisema.
Sababu za bajeti Wizara ya Afya kupungua
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 20, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment