Polisi wapigwa marufuku kufyeka mashamba ya bhangi


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amewapiga marufuku askari polisi kufyeka mashamba ya bhangi, kwani hiyo siyo kazi walioajiriwa kuifanya.

Rais Magufuli ametoa marufuku hiyo leo alipokuwa akihutubia wananchi waliofika kwenye sherehe za uzinduzi wa nyumba za askari polisi mkoani Arusha,  zilizofanyika uwanja wa Sheikh Amri Abeid, na kusema kwamba jambo hilo sio kazi yao.

Rais Magufuli ameendelea kwa kusema kwamba kazi ya kufyeka mashamba ya bhangi ni ya wenyewe wananchi wanaolima bhangi hizo, na iwapo hawatamkamata mhusika wa shamba, basi wasombe kijiji kizima kwenda kulifyeka.

“Ninyi hamkuajiriwa kwenda kufyeka mashamba ya bhangi, makamanda wako na maaskari wako, wasikate mashamba ya bangi, hawakuajiriwa kufyeka bhangi, tumieni njia za intelijensia wenu mtamshika tu, kama shamba lipo karibu na kijiji, shika kijiji kizima, wazee, wanawake, watoto, ndio wakafyeke hilo shamba la bhangi, ila IGP usiwatume maaskari wako kufyeka bhangi, mtaumwa nyoka mle, mna uniform nzuri msidhalilishe jeshi kwa kufyeka bhangi, mimi nisingefyeka bhangi, wa kufyeka wapo”, amesema rais Magufuli.

Rais Magufuli ameendelea kwa kusema kwamba kazi yao ni kuhakikisha nchi inakuwa salama, hivyo masuala kama hayo sio majukumu yao pia ni udhalilishaji kwa jeshi la polisi.

Polisi wapigwa marufuku kufyeka mashamba ya bhangi Polisi  wapigwa marufuku kufyeka mashamba ya bhangi Reviewed by KUSAGANEWS on April 07, 2018 Rating: 5

No comments: