Mapya yameendelea kuibuka katika
Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda baada ya wazazi wawili
kukutana ana kwa ana katika ofisi hizo
Kuanzia jana asubuhi, wanawake
waliotelekezwa na wenza wao walifurika katika ofisi ya RC Makonda kama
alivyoagiza ili kuwasaidia kisheria
Katika tukio la leo, Aprili 10,
mwanamke, Sylvia Felisiano alitinga katika viwanja vya ofisi ya RC Makonda,
baada ya kusikia mume wake amekwenda kulalamika kuwa amemkimbia na watoto wao
watatu
Awali, mwanaume, Tito Chembs,
alifika kwa mkuu wa mkoa akilalamika kuwa mke wake amempokonya watoto na kwenda
nao Bukoba
Saa chache baadaye, Sylvia alipata
taarifa hizo kupitia mitandao ya kijamii na kutinga katika ofisi hizo
Maofisa ustawi wa jamii waliokuwa
wakisikiliza mashauri hayo, waliwachukua wenza hao na kuingia nao ndani, huku
Sylvia akionekana mwenye hasira na kuahidi ataongea kwa kina na wanahabari
Mke, mume wakutana kwa Makonda
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 10, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment