Rais wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Dkt. John Pombe Magufuli leo Aprili 12, 2018
amewapandisha vyeo maafisa wa Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ)
katika vyeo mbalimbali na kumteua Kanali Bernard Masala Mlunga kuwa Mpambe wa
Rais (Aide de Camp – ADC).
Taarifa iliyosomwa na Mkuu wa
Majeshi ya Ulinzi Tanzania Jenerali Venance Salvatory Mabeyo, Ikulu Jijini Dar
es Salaam imeeleza kuwa Mhe. Rais Magufuli amempandisha cheo Meja Jenarali
Peter Paul Massao kuwa Luteni Jenerali.
Meja Jenerali Massao ni Mkuu wa Chuo
cha Mafunzo ya Maafisa Wanafunzi wa Jeshi Monduli (TMA) na kwa uteuzi huo, sasa
JWTZ itakuwa na Luteni Jenerali wawili.
Mhe. Rais Magufuli amempandisha cheo
Brigedia Jenerali Henry Kamunde kuwa Meja Jenerali.
Aidha, Mhe. Rais Magufuli
amewapandisha vyeo maafisa 27 wa JWTZ kutoka cheo cha Kanali na kuwa Brigedia
Jenerali na Afisa 1 kutoka Luteni Kanali na kuwa Kanali.
Kwa taarifa kamili soma hapa chini..
Hawa hapa waliopandishwa vyeo na JPM leo
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 12, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment