Katibu wa
Chadema, Kanda ya Iringa Mjini, Suzana Mgonokulima, ametangaza kumvua
uanachama aliyekuwa diwani wa chama hicho, Kata ya Gangilonga, Dady Igogo
Igogo pia
alikuwa Naibu Meya wa Manispaa ya Iringa
Katika taarifa
iliyotolewa leo Aprili 28, imeelezwa kuwa Igogo amevuliwa uanachama kwa kuwa
alikisaliti chama kwa kujivua nafasi ya unaibu meya na baadaye udiwani
“Ndugu Igogo
kwa muda mrefu amekuwa na mwenendo usioendana na itikadi, falsafa, madhumuni,
kanuni, maadili na sera za chama,” imesema taarifa hiyo
Taarifa hiyo
imesema kamati tendaji ya jimbo katika kikao chake cha dharura kilichoketi
Aprili 24 mwaka huu kiliadhimia Igogo avuliwe ujumbe wa kamati tendaji ya
jimbo, kwa kwenda kinyume na katiba ya chama kanuni na maadili
Taarifa hiyo
imeeleza kuwa Igogo amevuliwa uanachama kuanzia leo Aprili 28 kama
ilivyokubaliwa na wajumbe wa kamati.
Aliyekuwa Naibu Meya Chadema avuliwa uanachama
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 28, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 28, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment