KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI 8/3/2018 HAYA NDIYO BAADHI YA MAMBO YALIYOFANYWA NA JUMUIYA YA WANAWAKE MKOA WA ARUSHA CHINI YA MWENYEKITI YASMINI BACHU

Uongozi ni dhamana na unapopata lazima ujue unasimamia nini na unapomtaja mwanamke kuhusu uongozi kwa siku za nyuma watu walikuwa wanapuuza kwamba hawezi kuongoza watu bali familia yake Nyumbani.

Serikali imeweka Asilimia 50 kwa wanaume na 50 kwa wanawake ili wanawake wapate dhamana ya kusimama kwenye uongozi na ndicho kinachofanyika.

Tunapoelekea siku ya wanawake duniani ambayo kilele chake ni tarehe 8 mwezi 3 mwaka 2018 tumuangazie mwanamama ambaye ni mwenyekiti wa wanawake kwa mkoa wa Arusha Bi Yasmini Bachu ambaye alianza kazi rasmi tarehe 6/12/2017 mpaka sasa ni miezi mitatu baada ya kupewa dhamana ya kusimamia jumuiya ya wanawake UWT mkoa wa Arusha.

Alianza Kwa kufuatilia masuala yote yanayohusu miradi ya  jumuiya ya wanawake ngazi ya mkoa je kwanini hawanufaiki na mali zilizopo hasa viongozi wa UWT wilayani na wanawake wengine ndani ya mkoa wa Arusha mkoa wa Arusha unaundwa na wilaya za kichama saba ambazo ni Monduli,Karatu,Longido,(Arumeru )Arusha Dc +Meru ,Arusha Mjini,Ngorongoro.

Lakini safari hiyo ya kufuatilia mali za jumuiya ya Wanawake CCM ilianza akiwa na kamati yake ya utekelezaji yawanawake ya mkoa kufuatilia mguu kwa mguu miradi hiyo ya maduka yaliopo kata ya Kaloleni Maduka zaidi ya 72 ambayo kwa mwezi yanaingiza kiasi sha shilingi milioni 6 tu kwa kuwa kila duka linapangishwa kwa shilingi Elfu 80 licha ya kuwa yako mjini.

Maduka yaliyopo Levolosi zaidi  ya 75 ambayo kwa mwezi yanaipatia jumuiya shilingi milioni 6 laki 5 kwa kuwa chumba kimoja kinapangishwa kwa Shilingi Laki 1 ,ukijumlisha na maduka hayo ya kaloleni unapata Shilingi Milioni 12 na kiasi kadhaa kwa mwezina sehemu kubwa ya fedha hizo zilikuwa zikipokelewa mkononi ndani ya ofisi ya UWT mkoa na asilimia ndogo ndiyo zilipelekwa benki

Ikaanza safari nyingine ya kufuatilia vibanda vidogo vidogo vya Levolosi ambavyo wafanyabiashara wanavilipia shilingi 200 bila kujali ukubwa wake ambavyo ni zaidi ya 157 na wakati wote fedha zilikuwa zikilipwa mkononi kwenye ofisi ya UWT Mkoa bila kutolewa risiti halali (cash sale) utaratibu ambao fedha zote za makusanyo zilitakiwa ziingizwe benki kwa kuwa ndiyo utaratibu wa kifedha kwa taasisi kama hii.

Tunapozungumzia uwezo wa mwanamke kiongozi tunaona anavyotekeleza kile anachokiamini na kukisimamia kwa kuwa pia katiba ya UWT inamuongoza vyema .Mwenyekiti Yasmini Bachu alipiga marufuku maduka hayo yaliopo kaloleni na Levolosi kuitwa vibanda

“Katika hali ya kawaida maduka yaliyopo kaloleni yanatozwa elfu 80 na yale ya levolosi shilingi laki 1 je ni je ni sahihi kutoza viwango hivi kwa maeneo hayo yaliyopo katikati ya jiji la Arusha? Je Maduka madogomadogo na mengine yaliopo nje ya halmashauri ya jiji la Arusha kama vile Nduruma ,Bwawani Ngarenanyuki  na kadhalika yatatozwa viwango gani vya kodi ? Alihoji Yasmini Bachu

Katika Ziara hiyo Bi Yasmini Bachu pamoja na kamati yake walishuhudia upangaji juu ya Upangaji (Maduka yamepangishiwa watu wengine tofauti na Yule anayejulikana kwa mfano mtu x amempagishia mtu y kiasi cha shilingi laki 3 lakini anapeleka ofisi za umoja wa wanawake Uwt Shilingi elfu 80 au laki 1) sasa je kama fedha hiyo ingekuwa inapelekwa moja kwa moja UWT Mkoa mapato yangekuwa kiasi gani kwa Mwezi na kwa miaka kadhaa nyuma?

Baada ya ziara ya kutembelea maduka hayo na kujionea hali halisi kamati ya utekelezaji mkoa ilifanya mkutano na kuitisha wapangaji wote wa maeneo hayo mnamo tarehe 13/2 /2018 na kukubaliana  na wapangaji hao mambo mbalimbali ikiwemo usafi na utunzaji wa maeneo yote ya upangishaji,mikataba rasmi kuanzia tarehe moja mwei wa 6 /2018 itakayokuwa na masharti mbalimbali ,Ongezeko la Kodi Kuanzia tarehe moja mwezi wa 6 pamoja na pesa zote kupelekwa  Bank ,madeni yote yakuanzia April hadi December 2017 yalipwe kufikia tarehe 28 mwezi 2 2018,Maduka yote yapimwe ukubwa na kodi mpya ilipwe kulingana na ukubwa stahili,Kuondoa kabisa suala la upangaji juu ya upangaji na Kodi zote ziwe zikilipwa Benki kabla ya tarehe 5 ya kila mwezi (Kwa kuwa mkataba utakuwa wa mwaka mmoja mmoja)
                     
Hata hivyo mapato yanatazamiwa kuongezeka zaidi ya mara mbili na nusu hadi tatu ya mapato yanayopatikana sasa hivi na jumuiya hii imejiwekea mpango mkakati unaogusa mambo mbalimbali yatayotekelezwa kufikia december 2018 ikiwemo kuanza kupeleka fedha kila mwezi kwenye ofisi zote za UWT kwenye wilaya zote saba za Kichama kuanzia mwezi huu.Jambo ambalo halijawahi kufanyika kwa miaka zaidi ya 15 iliyopita

Kutokana na hali halisi kamati ya utekelezaji mkoa imeomba chama/Uwt Makao makuu ukaguzi maalum ufanyike kwenye miradi /mapato yake angalau kwa miaka miwili iliyopita.

Cha kujiuliza mimi na wewe ndugu msomaji wa makala hii inayoeleza namna kiongozi mwanamke anavyoweza kusimama katika nafasi yake na mabadiliko chanya  yakaonekana

Mwenyekiti na kamati ya utekelezaji mkoa wa Arusha wameanza program maalum tarehe 28 mwezi wa februari ya kuwafikia makundi makubwa ya wanawake walio na vipato vya hali ya chini kabisa wanaofanya biashara ndogondogo za mamalishe na mbogamboga waliopo masokoni na minadani ambao ni zaidi ya asilimia 80 ya wafanyabiashara wote wa maeneo hayo Lengo kubwa ni kujua kero na changamoto zote wanazokutana nazo kwenye maeneo yao ya biashara na wao kama wazalishaji wakuu na wanaotegemewa na familia
 Vile vile kuona malengo ya serikali ya awamu ya tano chini ya Mh Raisi Dokta Magufuli yanafikiwa na hasa uboreshaji wa maeneo wanayofanyia biashara ,kuondoa ushuru usio na tija kwenye kundi hili kama ilivyoelekezwa kwenye ilani ya CCM 2015 -2020

Pamoja na kujionea kama kundi hili wananufaika na zile asilimia 5 zinazotengwa na halmashauri kama mikopo nafuu kwa kundi la wanawake wajasiriamali wadogo zinawafikia program hii ni endelevu kufika masoko na minada mbalimbali ndani ya mkoa wa Arusha.
Ndugu msomaji haya yote ni uelekeo wa uongozi mpya chini ya Mwenyekiti wa Uwt Mkoa wa Arusha ambaye mpaka sasa ana siku 90 tu tangu alipokabidhiwa na kupewa dhamana ya kusimamia jumuiya ya Wanawake (UWT).

Ndugu Msomaji wa  makala hii kuanzia mwanzo lakini hakuna sehemu iliyomgusa mwanaume ambaye anaaminiwa kuwa ndiye mwenye nguvu na uwezo wa kuongoza lakini Tumemtaja mwanamke kuanzia mwanzo mpaka mwisho unapata picha kuwa nafasi ya mwanamke katika kutumikia jamii na kusimamia nafasi yake ni kubwa katika kuleta mabadiliko chanja .

Nikushukuru uliyetenga muda wako kusoma makala Hii imeandaliwa na kuletwa kwako name Alphonce Saul wa Kusaganewsblog Arusha



KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI 8/3/2018 HAYA NDIYO BAADHI YA MAMBO YALIYOFANYWA NA JUMUIYA YA WANAWAKE MKOA WA ARUSHA CHINI YA MWENYEKITI YASMINI BACHU KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI 8/3/2018 HAYA NDIYO BAADHI YA MAMBO YALIYOFANYWA NA JUMUIYA YA WANAWAKE MKOA WA ARUSHA CHINI YA MWENYEKITI YASMINI BACHU Reviewed by KUSAGANEWS on March 07, 2018 Rating: 5

No comments: