WATU WATATU CHADEMA WAPANDISHWA MAHAKAMANI



Wanachama  watatu wa Chadema wamefikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu na kuunganishwa na wenzake 28 wanaokabiliwa na shtaka la kufanya mkusanyiko isivyo halali.

Washtakiwa hao wamepandishwa kizimbani leo mbele ya Hakimu Mkazi Mwandamizi, Godfrey Mwambapa wakiwa na majeraha miguuni huku sehemu ya mapaja wakiwa wamefungwa bandeji
Wakili wa Serikali, Patrick Mwita amewasomea hati ya mashtaka inayowakabili washtakiwa hao watatu ambao ni Isack Ng'aga, Erick John na Aida Olomi.

Washtakiwa hao, Machi 8, 2018 wataunganishwa na wenzao 28 ambao ni Thabita Mkude, Haji Lukwambe, Emmanuel Kimoi, Mohammed Juma, Hussein Mrombo, Abdallah Hamis, Hussein Kidda, Paulo Kimoro, Brayan Morris, Hussein Nguli na Edna Kimoro
Wengine ni Jonathan Lema, Salha Ngondo, Ramadhan Mombo, Godwin Mwakasungura, Hassan Kibweda, Omary Hamad, Fatima Ramadhan, Ezekiel Nyenyembe, Denis Mtegwa, Dickson Kerefu, Raphael Mwaipopo, Athuman Mkawa, Mussa Kusigila, OMARY Danga, Jackson Masilingi, Asha Kileta na Ally Rajabu.

Kwa pamoja wanadaiwa Februari 16, 2018 katika eneo la Kinondoni Mkwajuni lililopo katika Wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam, walifanya mkusanyiko usio wa halali kinyume cha sheria.

Ilidaiwa kuwa mkusanyiko huo ulikuwa na nia ya kufanya uvunjifu wa amani na kusababisha taharuki kwa wananchi

Washtakiwa wote walikana shtaka hilo na wapo nje kwa dhamana kwa kila mshtakiwa kuwa na mdhamini mmoja ambaye alisaini ahadi ya Sh1.5 milioni na kutakiwa kutotoka nje ya Jiji la Dar es Salaam bila ya kuwa na kibali cha mahakama. 

Upelelezi bado haujakamilika.
Baada ya kuachiwa kwa washtakiwa hao watatu ndugu zao waliwakumbatia na kuangua vilio
WATU WATATU CHADEMA WAPANDISHWA MAHAKAMANI WATU WATATU CHADEMA WAPANDISHWA MAHAKAMANI Reviewed by KUSAGANEWS on February 28, 2018 Rating: 5

No comments: