Walimu 260 wafukuzwa kazi kutokana na makosa ya kinidhamu

Walimu 260 wamefukuzwa kazi mwaka 2016/17 kutokana na makosa mbalimbali ya nidhamu, ikiwamo utoro na kujihusisha na mapenzi na wanafunzi

Akizungumza katika mkutano wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TCD), katibu wake, Winfrida Rutahindurwa alisema Serikali haiwezi kuvumilia walimu wanaokiuka sheria, kanuni na taratibu za utumishi wa umma.
Rutahindurwa ambaye aliteuliwa kushika nafasi hiyo mwaka 2016, alisema alikuta mashauri 2,600 ya walimu mezani kwake yaliyokuwa yakihitaji ufumbuzi, huku asilimia 90 yakihusu utoro
“Utoro upo wa aina nyingi, kuna walimu wanadhani siku wakiwa hawana kipindi darasani wanaweza kulala nyumbani, wengine wanadhani wanafunzi wakiwa likizo na walimu wapo likizo, hii si sawa na sheria lazima ichukue mkondo wake,” alisema.
Katibu huyo alisema utoro mwingine ni baadhi ya walimu kwenda masomoni bila ruhusa ya wakuu wao wa vituo na wengine kujiongezea likizo ya masomo
Alisema sheria ya utumishi wa umma ipo wazi, mtumishi asipoonekana katika kituo chake cha kazi kwa siku tano mfululizo bila mwajiri wake kuwa na taarifa anapaswa kufukuzwa kazi
“Walimu ni sawa na watumishi wengine wa kawaida wa Serikali ambao likizo yao ni siku 28 kwa mwaka, hivyo wanapaswa kutambua kuwa likizo ya wanafunzi haiwahusu,” alisema.
Mapenzi shuleni Mkurugenzi wa Idara ya Ajira na Utumishi wa TCD, Christina Happe alisema licha ya makosa ya utoro na mapenzi shuleni, kuna tatizo la walimu kugomea uhamisho
“Uhamisho si uonevu bali ni taratibu za kawaida za kazi, hivyo mtumishi akihamishwa lazima aripoti kwanza kituo kipya cha kazi kama ana hoja za msingi za kuzuia uhamisho aziwasilishe,” alisema Happe.
Naye mwenyekiti wa tume hiyo, Oliver Mhaiki alisema kazi kubwa ya tume ni kusimamia maadili na nidhamu ya walimu, ikiwamo kutoa adhabu kwa wanaokwenda kinyume na sheria za utumishi.
Walimu 260 wafukuzwa kazi kutokana na makosa ya kinidhamu Walimu 260 wafukuzwa kazi kutokana na makosa ya kinidhamu Reviewed by KUSAGANEWS on February 27, 2018 Rating: 5

No comments: