Wanaume wanajali mavazi yao pia, sio wanawake tu.
Ila, mwanaume anabidi aelewe kwamba badala ya kufuata
mitindo, kupendeza kwenye tukio lolote kuna nguo ambayo utaihitaji. Nguo hizi
ni kama:
1. T-Shirt ya Pamba
Ukitaka t-shirt itakayo dumu kwa muda mrefu, nunua t-shirt
zilizotengenezwa kwa pamba tu. Pia, kuwa na t-shirt kadhaa zenye rangi tofauti,
zikiwemo:
· Za rangi ya kawaida kama Nyeupe, nyeusi, rangi ya kijivu
· Za rangi kali kama Njano, bluu nyepesi na kijani
Uzuri wa t-shirt ni kwamba zinaweza kuvaliwa na chochote
kile. Kwa hiyo, kuwa na aina nyingi kabatini.
2. Polo Shirts
Mwanaume yoyote anatakiwa kuwa na Polo Shirt (t-shirt zenya
kola) kadhaa. Zinafaa sana kuvaliwa kazini kwenye siku za Ijumaa au weekend.
3. Mashati ya kawaida
Mashati ya kawaida, ya mikono mirefu au mifupi, ni mazuri
kuvaa na jinzi na viatu au raba. Pia, zipo za aina na rangi tofauti kwa hiyo
tafuta itakayokufaa.
4. Mashati ya shughuli/sherehe rasmi
Kutegeamea na ajira yako, shati ya aina hii inaweza ikawa
nguo utakayoishia kuvaa kuliko zote. Kwa hiyo, lazima uwe nazo za kutosha za
aina mbalimbali.
Pia hata kama huzihitaji kwa kila siku, utazihitaji kwa
sherehekama harusi au mkutano mkubwa wa kikazi.
Muhimu kuliko vyote ni kuhakikisha unajua saizi yako na
kwamba unavaa shati linalo kutosha vizuri kabisa. Zaidi ya hapo, fikiria tai
utakayoivalia.
5. Bukta
Kwa kuzingatia joto lote la Tanzania, bukta ni muhimu.
Kuna aina nyingi za bukta na zenye rangi tofauti. Zinaendena
na polo shirt pamoja na viatu vya kawaida. Ni mazuri kuvaa kwenye wikiendi
ukiwa umetulia na washkaji.
6. Suruali za kawaida
Suruali za aina hii zina faraja na zinavaliwa kwenye
mazingira mbalimbali. Pia, kama polo shirt zinapatikana kwa rangi nyingi kwa
hiyo zinaweza kuvaliwa na mashati, viatu, kodia n.k za ain nyingi.
7. Jinzi
Jinzi zinaweza kuvaliwa kokote, siku yoyote.
Iwe ijumaa kazini au jumamosi usiku, hata kazini kwenye siku
ya kazi (kutegemea na masharti ya kazini kwako), jinzi zitavaliwa tu. Zipo za
aina nyingi, rangi tofauti na zinavaliwa na chochote kile.
Ila, ni muhimu kujua saizi yako ile upendeza unavyostahili.
Pia, jinzi zenye ubora zitakuwa na bei zaidi ila bora ununue jinzi yenye ubora
itakayodumu kwa miaka kuliko jinzi isiyo na ubora itakyodumu kwa miezi.
8. Koti la suti
Mwanaume yoyote anatakiwa kuwa na koti za suti za rangi ya
bluu na kijivu kabatini. Rangi hizi zinaendana na sherehe rasmi na zisizo
rasmi, na zinavaliwa na aina mbalimbali ya mashati na viatu.
Ila, muhimu zaidi ya rangi ni saizi. Hakikisha unajua saizi
yako na kwamba koti zinakutosha vizuri.
9. Chupi na Soksi
Hakikisha chupi zako ni nzuri, zinakutosha na ni safi (usije
ukajiaibisha). Kama zimechakaa, zitupe.
Soksi nazo ni vilevile. Ila, unahitaji kuwa na aina tofauti
za soksi kwa ajili ya mavazi tofauti. Hakikisha rangi ya soksi zako zina ukali
au ni nzito kidogo ya suruali yako.
10. Viatu
Kwa kawaida, viatu ni vitu vya kwanza vya mtu kuangalia
akikuona, hasa na wanawake. Kwa, sio swala la kupuuzia.
Cha muhimu ni kwamba ni visafi na ziko katika hali nzuri.
Muungwana anarahisisha mambo
Ndio, inabidi ujaribu nguo mbalimbali ila ujue
kinachokupendeza. Ila, kuwa na mavazi yasiyo na mbwembwe nyingi si mbaya.
Bahati nzuri, nguo tulizoorodhesha hapo juu zitakusaidia kupendeza bila kuweka
juhudi saaaaana.
Jua Mavazi Muhimu kwa Wanaume Tanzania
Reviewed by KUSAGANEWS
on
February 27, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
February 27, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment