VITUO 57 VYA MAFUTA VYAFUNGIWA ARUSHA KWA KUKOSA MASHINE ZA EFD,s

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) mkoani Arusha imevifungia vituo 57 vya kuuza dizeli, petroli na mafuta ya taa kutokana na kutokuwa na mashine za kielektroniki za kutoa risiti (EFDs).

Akizungumza na Kusaga News juu ya hatua hiyo Meneja wa Mamlaka hiyo mkoani Arusha Bwana Apili Mbaruku amesema vituo hivyo vipo katika Wilaya za Arusha mjini; Karatu; Monduli; Arumeru; Loliondo pamoja na Longido.

Ameongeza kuwa waliochelewa kufunga hizo mashine za kielektroniki za kutoa risiti (EFDs); adhabu yao ni kati ya shilingi milioni tatu na milioni nne.

Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi  wa TRA Richard Kayombo amesema  kwamba  wanaendelea na kazi hiyo nchi nzima ili kuhakikisha sheria inatekelezwa.


VITUO 57 VYA MAFUTA VYAFUNGIWA ARUSHA KWA KUKOSA MASHINE ZA EFD,s VITUO 57 VYA MAFUTA VYAFUNGIWA ARUSHA KWA KUKOSA MASHINE ZA EFD,s Reviewed by KUSAGANEWS on July 15, 2017 Rating: 5

No comments: