MTU MMOJA AUWAWA KIKATILI KUTOKANA NA MGOGORO WA WAKULIMA NA WAFUGAJI MKOANI RUKWA



Mtu mmoja ambaye ni mfugaji ameuawa kikatili na kundi la watu wenye hasira kali wa kijiji cha Kifone katika kata ya Mwimbi wilaya ya Kalambo mkoani Rukwa, baada ya kutokea kutoelewana kati ya wakulima na wafugaji.

Ukatili huo umetokea kufuatia kundi la Ngombe kuachiliwa kuingia kwenye mashamba ya wakulima na kuharibu kiasi kikubwa cha mazao jambo lilizua taharuki ndipo kupelekea kifo cha mfugaji huyo.

Akizungumza  diwani wa kata ya Mwimbi Claudio Mweupe, wamesema licha ya mfugaji huyo kuuawa kikatili kwa kukatwa katwa na mapanga, lakini na mwenziwe naye Rehi Mwandu amejeruhiwa vibaya baada ya kushambuliwa na kundi hilo la wakulima,

Mpaka sasa majeruhi  amelazwa kwenye hospitali ya rufaa ya mkoa wa Rukwa mjini Sumbawanga, huku msako mkali ukiendelea kuwatafuta watu wote waliohusika na kitendo hicho cha kujichukulia sheria mkononi.

Mkuu wa wilaya ya Kalambo Julieth Binyura, akiongea kwenye kijiji hicho cha Kifone akiwa ameongozana na kamati ya ulinzi na usalama ya mkoa chini ya mwenyekiti wake Bw Zelote Steven, amesema tayari wameanza kuwashikilia viongozi wa vijiji na vitongoji wanaoruhusu makundi ya Ngombe kuingia kwenye maeneo yao.
MTU MMOJA AUWAWA KIKATILI KUTOKANA NA MGOGORO WA WAKULIMA NA WAFUGAJI MKOANI RUKWA MTU MMOJA AUWAWA KIKATILI KUTOKANA NA MGOGORO WA WAKULIMA NA WAFUGAJI MKOANI RUKWA Reviewed by KUSAGANEWS on November 13, 2016 Rating: 5

No comments: