MAHAKIMU WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI ILI KUTENDA HAKI


Jaji kiongozi wa mahakama kuu ya Tanzania  Ferdinand Wambali

Jaji kiongozi wa mahakama kuu ya Tanzania  Ferdinand Wambali amewataka mahakimu katika ngazi zote hapa nchini kutoa maamuzi ya mashauri yanayofikishwa mbele yao kwa kuzingatia viapo vya taaluma yao na ushahidi unaotolewa mahakamani ili waweze kuheshimika ndani ya jamii.

Mheshimiwa Wambali ambaye yuko mkoani Kagera kwa ajili ya ziara ya siku moja amesema mtumishi wa idara ya mahakama ataheshimika endapo atatoa huduma nzuri kwa wananchi hivyo mewataka wafanye kazi yao kwa kujiamini, kitaaluma na kwa uaminifu mkubwa.

Baadhi ya watendaji wa mahakama wamesema wameiomba idara ya mahakama iwaondoe washauri wa baraza kwenye mfumo wa mahakama za mwanzo katika kutoa maamuzi.

Naye mtendaji wa mahakama kuu Tanzania Solanus Nyimbi amesema ufinyu wa bajeti  ndio unakwamisha baadhi ya mipango ya idara ya mahakama.
MAHAKIMU WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI ILI KUTENDA HAKI MAHAKIMU WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA WELEDI ILI KUTENDA HAKI Reviewed by KUSAGANEWS on November 13, 2016 Rating: 5

No comments: