Idadi
ya Watumishi hewa wameendelea kuongezeka mkoani arusha baada ya oparesheni
inayoendelea kuwasaka hao katika maeneo mbalimbali ndani ya wilaya za mkoa wa
arusha.
Akizungumza
na GUMZO TZ mkuu wa mkoa wa Arusha Daudi Felix Ntibenda amesema kuwa idadi hiyo
ya watumishi hewa imeongezeka kutoka watumishi hewa 270 mpaka 320 kufikia hivi
sasa nab ado oparesheni ya kubaini wengine inaendelea.
“mpaka
leo hii nimetuma kamati yangu maalum ya kushughulikia watumishi hewa na
tunaendelea kuwabaini kila siku na tuko makini katika kuhkikisha tunawabaini
wote na kuwashughulikia kwa uhakika”alisema
Ntibenda
ameongeza kwamba wanapokamatwa watumishi hewa na kubainika lazima walipe pesa
zote walizo tumia na kasha sheria ifuate mkondo wake na kuwaburuza mahakamani
haraka iwezekanavyo.
Na
amesisitiza kwamba mtumishi hewa atakapobainika atabanwa mpaka aseme nani alimuajiri na kushughulikia na
wote kuchukuliwa sheria zaidi na hili likiwa ni agizo maalum kutoka kwa raisi
ambalo mpaka sasa linatekelezwa.
Mkoa
wa Arusha mpaka sasa unaongoza kwa kufanya vizuri katika zoezi la kubaini
watumishi hewa na kwa mujibu wa mkuu wa mkoa amesema huenda wakaongezeka zaidi
kwasababu zoezi hilo bado ni endelevu.
“Na
mpaka sasa watumishi hewa hao wanahaha na wameshanza kurudisha fedha na wengine
wameshahama hata wizara zao nawengine kukimbia lakini tutawabaini tu”alisema
MKUU WA MKOA WA ARUSHA ABAINI WATUMISHI HEWA WENGINE AMBAO WAMEONGEZEKA SASA KUTOKA 270 MPAKA 320
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 13, 2016
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 13, 2016
Rating:


No comments:
Post a Comment