Trump afichua mchepuko wake

Rais wa Marekani Donald Trump amekiri kuwa alirejesha fedha kwa wakili wake baada ya kumlipa nyota wa filamu za ngono Stormy Daniels ili kumzuia kufichua uhusiano wao. 

Ofisi ya Maadili ya Serikali ya Marekani imegundua kuwa Trump huenda alifichua malipo hayo akitangaza matumizi ya fedha awali.

Matumizi hayo ya fedha yanaonyesha kuwa alimlipa Michael Cohen kwa matumizi ya fedha ya mwaka 2016 kati ya dola 100,001 na 250,000.

Malipo kwa Stormy Daniels yanaweza kuwa tatizo la kisheria kwa Rais Trump kwa sababu yanaweza kuonekana ni matumizi mabaya ya pesa za kampeni.
Trump afichua mchepuko wake Trump afichua mchepuko wake Reviewed by KUSAGANEWS on May 17, 2018 Rating: 5

No comments: