Mkurugenzi wa jiji la Arusha Akabidhiwa Vyoo kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa kuona


Mkurugenzi wa jiji la Arusha Athumani Kihamia na Mkurugenzi wa shule ya msingi Upendo Friends Bi Isabela Mwampamba wakiwa katika picha ya pamoja na watoto wenye ulemavu wa macho leo wakati wakikiabidhiwa vyoo vya matundundu sita shule ya msingi Themi jiji la Arusha
Walimu wakiwa na watoto wa shule ya msingi Themi  wenye ulemavu wa macho wakiwa wamekaa kwenye hafla ya kukabidhiwa vyoo na mkurugenzi wa Shule ya Upendo Friends
Mkurugenzi wa jiji la Arusha Athumani Kihamia na Mkurugenzi wa Shule ya Upendo Friends leo katika tukio la kukabidhi vyoo vya wanafunzi wenye ulemavu wa kuona
Wanafunzi wa Shule ya msingi Themi jiji la Arusha
Wanafunzi wenye ulemavu wa kuona wakiimba wimbo katika hafla ya leo katika shule ya msingi Themi 
Mkurugenzi wa Shule ya msingi Upendo Friends Bi Isabela Mwampamba akisema jambo katika hafla ya leo
Mkurugenzi wa Shule ya Upendo Friends Bi Isabela Mwampamba amekabidhi vyoo 6 vya kisasa vyenye dhamani ya Shilingi milioni 22.5 kwa ajili wanafunzi wenye ulemavu wa kuona katika shule ya msingi Themi iliyoko katika jiji la Arusha.


Akimkabidhi mkurugenzi wa jiji la Arusha Vyoo hivyo Bi Isabela amesema kuwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwemo CRDB BANK,Bulk Distributor na wengineo wamefanya hivyo kwa lengo la kuwasaidia wanafunzi hao ambao wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya sehemu kwa ajili ya Kujisitiri.

Amewahamasisha wadau wengine mbalimbali kuguswa na kujitoa kuwasaidia wenye uhitaji maalumu;kwa kuwa yeye pamoja na wenzake wamekuwa mfano.


Mkurugenzi wa jiji la Arusha Athumani Juma Kihamia ameshukuru kwa msaada huo, na kusema kwamba Mama Isabela anatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi CCM kwa kuwa ilani ndiyo inayoongoza shughuli za serikali na kuwenye ilani imeeleza kwamba serikali itashirikiana na wadau mbalimbali kutatua changamoto za kijamii.

Mwalimu mkuu wa shule hiyo Zebedayo Moleli amesema vyoo hivyo ni msaada mkubwa kwa watoto hao kwani vitawasaidia kuepuka magonjwa ya mlipuko kutokana na changamoto inayowakabili.


Mkurugenzi wa jiji la Arusha Akabidhiwa Vyoo kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa kuona Mkurugenzi wa jiji la Arusha Akabidhiwa Vyoo  kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa kuona Reviewed by KUSAGANEWS on March 08, 2018 Rating: 5

No comments: