Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu
(LHRC) kimeitaka Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) kufanyia kazi changamoto
zilizoibuliwa na wadau wakati wa uchaguzi mdogo wa ubunge Kinondoni na Siha
bila kujali udhaifu katika uwasilishaji wa changamoto hizo
Kituo hicho kimedai kuwa kuibuliwa
kwa changamoto hizo kunalenga kujenga jamii yenye haki na usawa.
yameelezwa leo Jumatano Machi 7,
2018 na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa LHRC, Naemy Sillayo alipokuwa akijibu hoja
zilizotolewa na NEC wiki iliyopita kutokana na tamko lililotolewa na asasi za
kiraia
Sillayo amesema tamko hilo
halikutolewa na LHRC bali lilitolewa na umoja wa asasi za kiraia ambao kituo
hicho ni mwanachama.
Sillayo amesema LHRC inakubaliana na
hoja iliyotolewa na azaki ya kutaka NEC kuboresha kanuni za usimamizi wa
uchaguzi na kutovibana vyombo vya habari
“Hilo litasaidia kutoweka mipaka kwa
vyombo vya habari wakati wa kutimiza jukumu la kutoa taarifa kwa umma,"amesema.
LHRC kwa NEC kufanyia kazi changamoto walizotaja
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 07, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 07, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment