Mahakama ya Hakimu Mkazi Mbeya
imewatia hatia mbunge wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi maarufu Sugu na Katibu wa
Chadema Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Emmanuel Masonga
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya
Hakimu Mkazi Mbeya, Michael Mteite aliyeanza kusoma hukumu leo Februari 26,2018
saa 03:32 asubuhi amesema washtakiwa wana hatia kwa makosa waliyoshtakiwa.
Baada ya kuwatia hatiani washtakiwa,
hakimu Mteite anasubiriwa kutamka adhabu dhidi yao.
Sugu na Masonga wanashtakiwa kwa
kosa la kutumia lugha ya fedheha dhidi ya Rais John Magufuli.
Wawili hao wanadaiwa kutenda kosa
hilo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika Desemba 30,2017 eneo la Uwanja wa
Shule ya Msingi Mwenge jijini Mbeya.
HAKIMU ANASUBIRIWA KUTAMKA ADHABU YA SUGU NA KATIBU WA CHADEMA
Reviewed by KUSAGANEWS
on
February 26, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment