Muda ulipaji kodi ya majengo waongezwa hadi Julai 31



Wakati leo ndiyo ilikuwa tarehe  ya mwisho wa ulipaji wa kodi za majengo ya mwaka 2016/2017, Mamlaka ya Mapato nchini (TRA) imesogeza mbele zoezi hilo hadi Julai 31.

Akizungumza  Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipakodi, Richard Kayombo amesema uamuzi huo umefikiwa baada ya kuona bado kuna watu wengi wanahitaji kulipia kodi hiyo

Amesema kwa Jiji la Dar es Salaam zimetengwa ofisi maalumu kwa ajili ya kazi hiyo hiyo ili kutoa fursa kwa ofisi nyingine kuendelea kukusanya kodi nyingine

Kwa muda mrefu kidogo wahudumu wa TRA wamejikita zaidi kwenye kodi ya majengo, sasa tumeona tutenge maeneo maalumu ili wanaolipa kodi nyingine nao waendelee kuhudumiwa kwa ufanisi," amesema

Ofisi zitakazoendelea na zoezi hilo kwa Dar es Salaam ni TRA Mbagala, Temeke, Kigamboni, Kimara, Tegeta, Manzese, Ilala, Gerezani, Vingunguti, Samora, Kijitonyama na ofisi ya TRA ndani ya viwanja vya Sabasaba.

Kayombo amesema baada ya Julai 31 watakaolipa kodi hiyo wataambatanisha na faini.
Muda ulipaji kodi ya majengo waongezwa hadi Julai 31 Muda ulipaji kodi ya majengo waongezwa hadi Julai 31 Reviewed by KUSAGANEWS on July 15, 2017 Rating: 5

No comments: