Watu kadhaa wamejeruhiwa kufuatia ajali iliyotokea asubuhi ya leo, Jumamosi, Julai 22, baada daladala aina ya coaster kuigonga treni maeneo ya Tandika.
Mashuhuda waliokuwepo eneo la tukio wamedai kuwa kuna majeruhi kadhaa ambao wamenza kufanya jitihada za kuwaokoa kutoka katika gari hilo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Temeke, Gilles Muroto amezungumza na Mwananchi kwa njia ya simu na kuthibitisha ajali hiyo.
Muroto amesema bado hana taarifa ya uhakika juu ya ajali hiyo na atazungumza pindi atakapofika sehemu ajali ilipotokea.
“Ni kweli ajali imetokea ila sina taarifa sahihi hadi nikifika, ndiyo naelekea,” amesema Muroto.
Coaster yagonga treni leo
Reviewed by KUSAGANEWS
on
July 22, 2017
Rating:

No comments:
Post a Comment