![]() |
| kamanda wa polisi mkoa wa kilimanjaro Wilbroad Mtafungwa |
Polisi mkoani Kilimanjaro, imetia mbaroni mtu anaedaiwa
kumkata mwanamke mmoja mkazi wa chekereni, maziwa yote mawili, baada ya kukataa
kufanya nae mapenzi.
Akidhibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro Wilbroad Mutafungwa, amesema mtuhumiwa huyo anayefahamika kwa jina la Arnold Josephat, amekamatwa jana Juni 29 mwaka huu,majira ya usiku, baada ya jeshi hilo kupata taarifa kwa raia wema,kuwa mtuhumiwa huyo ameingia kwa siri, kijiji hapo.
Kamanda amesema tukio la kukatwa matiti kwa mwanamke huyo aitwae Mary Aloyce Lyimo, (23), mkazi wa Chekereni, wilaya ya Moshi, lilitokea Februari 7, mwaka huu,ambapo mtuhumiwa baada ya kufanya tukio hilo alikimbia.
Akielezea mazingira ya tukio hilo, Kamanda amesema siku ya tukio, kijana huyo alimtokea mwanamama huyo nyumbani kwake,huku akiwa ameshika panga mkononi na kutaka kufanya nae mapenzi kwa lazima, lakini alipokataa ndipo alipomvua nguo kwa nguvu, na kumkata maziwa yote mawili, kisha kuyaweka kwenye mfuko wa malboro na kuondoka nayo.
Amesema Juni 29, mwaka huu usiku, polisi walipata taarifa ya kuwa mtuhumiwa huyo ameonekana maeneo ya kijijini hapo na ndipo wapeleleziwalipokwenda na kufanikiwa kumtia mbaroni.
Aidha amesema kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo,kutasaidia kuimarisha uchunguzi wa jeshi hilo ambao ulikuwa unaendelea tangu kutokea kwa tukio hilo, na kwamba baada uchunguzi huo, mtuhimiwa huyo atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo.
Akidhibitisha kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro Wilbroad Mutafungwa, amesema mtuhumiwa huyo anayefahamika kwa jina la Arnold Josephat, amekamatwa jana Juni 29 mwaka huu,majira ya usiku, baada ya jeshi hilo kupata taarifa kwa raia wema,kuwa mtuhumiwa huyo ameingia kwa siri, kijiji hapo.
Kamanda amesema tukio la kukatwa matiti kwa mwanamke huyo aitwae Mary Aloyce Lyimo, (23), mkazi wa Chekereni, wilaya ya Moshi, lilitokea Februari 7, mwaka huu,ambapo mtuhumiwa baada ya kufanya tukio hilo alikimbia.
Akielezea mazingira ya tukio hilo, Kamanda amesema siku ya tukio, kijana huyo alimtokea mwanamama huyo nyumbani kwake,huku akiwa ameshika panga mkononi na kutaka kufanya nae mapenzi kwa lazima, lakini alipokataa ndipo alipomvua nguo kwa nguvu, na kumkata maziwa yote mawili, kisha kuyaweka kwenye mfuko wa malboro na kuondoka nayo.
Amesema Juni 29, mwaka huu usiku, polisi walipata taarifa ya kuwa mtuhumiwa huyo ameonekana maeneo ya kijijini hapo na ndipo wapeleleziwalipokwenda na kufanikiwa kumtia mbaroni.
Aidha amesema kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo,kutasaidia kuimarisha uchunguzi wa jeshi hilo ambao ulikuwa unaendelea tangu kutokea kwa tukio hilo, na kwamba baada uchunguzi huo, mtuhimiwa huyo atafikishwa mahakamani kujibu tuhuma hizo.
Katika tukio lingine,jeshi la polisi mkaoni Kilimanjaro, linafanya
uchunguzi kuhusiana na tukio la wasichana wawili kukeketwa, wakati tayari serikali ilishapiga marufuku vitendo hivyo viovu.
Kamanda wa polisi mkoani hapa, Wilbroad Mutafungwa, amesema wasichana hao ambao majina yao yanahifadhiwa kutokana na umri wao kuwa mdogo, waligundulika kufanyiwa vitendo hivyo baada ya walimu wao kuwaona wakitembea isivyokawaida.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na polisi,juni 22 mwaka huu,
wasichana hao wanaoishi kijiji cha Sanya Stesheni, wilayani Hai,
walichukuliwa shuleni wanakosama, ambapo ni shule ya Msingi Obran, na Baba yao mkubwa kwa kuomba ruhusa kuwa wanakwenda kwenye Ubarikio.
Amesema baada ya kuchukuliwa na baba yao mkubwa, walipelekwa kijiji cha Lengasiti Wilaya ya Simanjiro mkoani Manyara, na kesho yake, wakiwa kijijini humo, wanawake wawili walifika na kuwachukua kwa nguvu na hatimae kuwakeketa.
Kamanda amesema baada ya tukio hilo, walirudi shuleni
wakiwa katika hali hiyo hadi pale walimu wao walipoigundua hali yao, na kutoa taarifa
hiyo polisi.
Aidha amesema kwa kuwa tukio hilo lilitokea eneo la Lengasiti, wilaya Simanjiro, jeshi la polisi mkoani humo linaanda jalada na kulipeleka mkoani Manyara kwa ajili ya uchunguzi zaidi.
MTU MMOJA AKAMATWA KWA KUMKATA MATITI MWANAMKE KILIMANJARO
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 30, 2016
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
June 30, 2016
Rating:


No comments:
Post a Comment