MCHUNGAJI WA KANISA AMBAKA MTOTO WA MIAKA 17 ARUSHA



Jeshi la polisi mkoani Arusha linamshikilia Mchungaji wa Kanisa la Victory lililopo Sokoni One CHRISANTUS MBOYA kwa tuhuma za kumbaka msichana mwenye umri wa miaka 17 aliye na matatizo ya kiafya kwa muda mrefu ambaye anaishi na Dada yake eneo la Moshono mkoani hapa.

Akizungumza na vyombo vya habari Kwa niaba ya kamanda wa polisi   Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Arusha Kamishina msaidizi mwandamizi wa polisi Yusuph Ilembo amesema tukio hilo June 3 mwaka huu saa nne asubuhi katika eneo la Sokoni One nyumbani kwa mchungaji huyo wakati mke wake akiwa hayupo.

Amesema Msichana huyo ni muumini katika Kanisa hilo na kutokana na hali yake ya afya mchungaji huyo aliitumia fursa hiyo kumwita kwenda nyumbani kwake ili akamfanyie maombi kwa madai kwamba alikuwa amelishwa sumu na wachawi na alipokwenda badala ya kumfanyia maombi alimbaka.

Amesema baada ya kitendo hicho mchungaji huyo alimwambia asimwambie mtu yeyote; ambapo June 10 majira ya saa tano asubuhi dada yake alichukua simu ya msichana huyo na kuuona ujumbe uliotoka kwenye simu ya mchungaji huyo wa kumwomba radhi kwa kitendo kilichofanyika.

Kamanda Ilembo ameongeza kuwa baada ya msichana huyo kuhojiwa alieleza yote yaliyotokea na ndipo taarifa zikapelekwa katika kituo kikuu cha polisi Arusha kwa hatua zaidi;na kwamba kutokana na afya ya msichana huyo alipewa PF3 na kwenda hospitali ya Mount-Meru ambako amelazwa kwa uchunguzi zaidi.
MCHUNGAJI WA KANISA AMBAKA MTOTO WA MIAKA 17 ARUSHA MCHUNGAJI WA KANISA AMBAKA MTOTO WA MIAKA 17 ARUSHA Reviewed by KUSAGANEWS on June 12, 2016 Rating: 5

No comments: