Mkenya atimuliwa kwa sababu ya rangi


 Mchezaji gofu ya kulipwa nchini Kenya‬ ametimuliwa mashindanoni baada ya kufoka kwenye mtandao wake wa Facebook kuwa alikuwa amebaguliwa kwa msingi ya rangi yake katika klabu ya gofu ya Karen.
\
Hatua hiyo imezua mjadala mkubwa miongoni mwa wapenzi wa gofu baada ya kudai kuwa alibaguliwa kwa misingi ya rangi yake katika klabu ya gofu ya Karen.
Kupitia mtandao wake wa Facebook Richard Ainley aliwaambia wafuasi wake kuwa alikuwa amebaguliwa alipokuwa akitaka kuegesha gari lake
kabla ya kushiriki mkondo wa kwanza wa mchuano wa Gofu ya kimataifa ya Kenya Open ulioanza mapema leo.

Mashindano hayo yanayoandaliwa kila mwaka ni sehemu ya ligi ya kimataifa ya gofu ya European tour.
Ainley alisema ''Looooo kumbe ukoloni bado upo Kenya !''
''Nimelazimika kutembea mwendo mrefu nikikokota gari langu la vigongo baad ya kunyimwa ruhusa ya kuegesha gari langu

ndani ya klabu ya gofu ya Karen licha ya kuwa mimi ni mkenya naambiwa kuwa ni Wazungu na waafrika wachahe tu wanaoruhusiwa kuingia humu''
hawajui kuwa mimi ni mchezaji wala hawataki kujua.
''Shindwe !Kwa hakika imenikera sana '' alifoka Ainley

Muda mchache baadaye Ainley aliitwa katika afisi za mwendesha mashindano wa klabu hiyo na kuelezwa kuwa alikuwa amekiuka sheria maadili na ustaraabu
wa klabu hiyo ya Karen na hivyo hatoruhusiwa kuendelea na mashindano.
''Nimekatazwa kuchezwa kwa sababu ukweli wa hali kama nilivyo andika awali katika mtandao wangu wa Facebook.
 .
Mkenya atimuliwa kwa sababu ya rangi Mkenya atimuliwa kwa sababu ya rangi Reviewed by KUSAGANEWS on April 09, 2015 Rating: 5

No comments: