RC TANGA ATOA MAAGIZO MAZITO NDANI YA WIKI MBILI AKUTE YAMETEKELEZWA/ DC KALIST LAZARO AYAPOKEA

Mkuu wa Mkoa wa Tanga ndugu Adam Kigoma Malima ametembelea na Kukagua Ujenzi wa Vituo vitatu vya Afya Wilayani Korogwe ambavyo ni Kituo cha Afya Mgombezi na Kwamsisi vilivyopo katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe na Kituo cha Afya Mnyuzi kilichopo katika Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe.

Akielezea Maendeleo ya Ujenzi wa Kituo cha Afya Mgombezi Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Ndugu Kalisti Lazaro alisema, "Mheshimiwa Mkuu wa Mkoa karibu katika Wilaya yetu ya Korogwe, hapa tulipoanzia Ziara yako ni Kituo cha Afya Mgombezi ambocho kilipokea fedha kiasi cha Tsh 250,000,000/= tarehe 08/06/2021 na Kituo cha Afya Kwamsisi ambacho kilipokea fedha kiasi cha Tsh 250,000,000/= tarehe 16/09/2021 na Kituo cha Afya Mnyuzi ambacho kilipokea fedha kiasi cha Tsh 250,000,000/= tarehe 20/10/2021. Mheshiwa Mkuu wa Mkoa kama unavyojionea hapa katika Kituo cha Afya Mgombezi Ujenzi upo katika hatua ya kutandika Jamvi na Kituo cha Afya Kwamsisi kipo kwenye hatua ya kusafisha eneo na kuweka Michoro kwa ajili ya kuanzia kuchimba Msingi na Kituo cha Afya Mnyuzi tayari wameshaanza kuchimba Msingi" aliongeza "... Mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Afya Mgombezi unakadiriwa kutumia Jumla ya Tsh 262,831,688 kwa Majengo yote Mawili, ambapo kiasi cha Tsh 122,789,438 kitatumika kwa Jengo la Upasuaji na Kiasi cha Tsh 140,042,250/= kwa Jengo la Wazazi na Mpaka sasa kiasi cha Tsh 11,394,609.75/= zimeshatumika mpaka sasa kwa hatua ya Ujenzi uliyofikiwa. Makadirio ya Ujenzi wa Kituo cha Afya Kwamsisi kwa Majengo Mawili ya mwanzo ni Tsh 171,394,791 kwa Jengo la OPD na Tsh 78,352,722 kwa Jengo la Maabara ambapo kwa sasa tayari Mafundi wameshaanza kuweka alama kwa ajili ya kuchimba Msingi na Kituo cha Afya Mnyuzi tayari wameshachimba Msingi wa Jengo moja la Wagonjwa wa nje (OPD)

Hata Hivyo Mh Malima hakufurahishwa na hatua iliyofikiwa katika Ujenzi wa Kituo cha Afya Mgombezi ambapo  amemuagiza Mkurugenzi wa Mji wa Korogwe ndugu Nicodemus J Bei kuwachukua Wanakamati wa Kituo cha Afya Mgombezi kwenda Kujifunza kwa wenzao wa Kituo cha Afya Sindeni - Handeni ambao wamefika kwenye hatua ya Kupaua.

Amesema  Vituo vyote hivyo viliingiziwa hela wakati mmoja na Mkuu wa Mkoa amesema atarudi baada ya tarehe 01/12/2021 (Wiki mbili na siku mbili) na akute Ujenzi upo kwenye hatua ya Kupaua na tarehe 01/01/2022 Ujenzi uwe umekamilika na Jengo likabidhiwe likiwa tayari kwani Mradi huu ni wa siku 90 tuu.

Katika Kituo cha Afya Kwamsisi Mkuu wa Mkoa amemuagiza Mkurugenzi wa Mji wa Korogwe baada ya wiki mbili atakuja na akute Msingi umeshakamilika, na atakuja tena na akute Ujenzi upo kwenye hatua ya Lenta, na atakuja tena baada ya wiki mbili tena 01/01/2021akute Ujenzi upo kwenye hatua ya Kupaua na tarehe 15/01/2022 atakuja Kufungua Kituo cha Afya na aliwataka Wananchi wa Kwamsisi kutoa Ushirikiano katika kulinda Vifaa vya Ujenzi vitakavyoletwa kwenye eneo la Mradi.

Katika Kituo cha Afya Mnyuzi Mkuu wa Mkoa alifurahishwa na Jitihada za Wananchi na alimuaguza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe kuwa Jengo linatakiwa likamilike tarehe 15/01/2021 na alihaidi siku ya Kufungua Jengo atatoa Ng'ombe na Mbunge wa Jimbo la Korogwe Vijijini Ndugu Timotheo Mzava alihaidi kutoa Mchele, huku Diwani wa Kata ya Mnyuzi ndugu Michael Mhina alihaidi kutoa Mbuzi na Mafuta na Mkuu wa Wilaya ya Korogwe alihaidi kutoa Maji na Soda Kufurahi na Kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuwaletea Mradi wa Kituo cha Afya na aliwaonya wale wote wanaozitolea macho Fedha za Miradi ya "Tozo" na "Mpango wa Maendeleo kwa Ustawi wa Taifa na Mapambano DHIDI ya UVIKO-19" kuwa Fedha za Miradi hiyo si za Kuchezewa na atashughulika na wote watakaobainika kukwapua Fedha hizo.



RC TANGA ATOA MAAGIZO MAZITO NDANI YA WIKI MBILI AKUTE YAMETEKELEZWA/ DC KALIST LAZARO AYAPOKEA RC TANGA ATOA MAAGIZO MAZITO NDANI YA WIKI MBILI AKUTE YAMETEKELEZWA/ DC KALIST LAZARO AYAPOKEA Reviewed by KUSAGANEWS on November 16, 2021 Rating: 5

No comments: