Ili kuepuka kile ilichodai kuwa ni hujuma nyakati za
uchaguzi, Chadema imepanga kuwatumia wabunge wake 19 kuwa mawakala katika Kata
ya Kizota jijini Dodoma
Wabunge hao watatumika katika Kata ya Kizota jijini Dodoma
kwenye uchaguzi utakaofanyika Septemba 16, ukihusisha pia kata 23 na majimbo
mawili ya ubunge. CCM imeshatangazwa mshindi katika kata tatu na jimbo moja la
Korogwe
Majimbo yatakayohusika katika uchaguzi huo mdogo ni Monduli
la Arusha na Ukonga jijini Dar es Salaam baada ya waliokuwa wabunge wake kupitia
Chadema, Mwita Waitara (Ukonga) na Julius Kalanga (Monduli) kutimkia CCM kisha
kupitishwa tena CCM kuwania nafasi hiyo
Kwa mujibu wa ratiba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC),
kampeni zilianza Jumatatu Agosti 21. Hata hivyo, si CCM wala Chadema
inayoshirikiana na ACT-Wazalendo waliozindua kampeni
Jana, Katibu wa Chadema Kanda ya Kati, Iddi Kizota
akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma muda mfupi baada ya mgombea wa
chama hicho, Omary Bangababo kurudisha fomu ya kugombea udiwani alisema
watawatumia wabunge kusimamia upigaji na kuhesabu kura
Alisema wamefikia uamuzi huo baada ya baadhi ya mawakala
wanaowekwa vituoni kujiondoa siku ya kupiga kura
“Ikiwezekana tutatumia hata wabunge na ukiangalia uchaguzi
unafanyika Septemba 16, 2018 kipindi ambacho Bunge linaendelea na vikao vyake
basi wabunge 19 tutaweza kuwapata,” alisema Kizota
“Katika kata yetu ya Kizota tuna vituo vya kupigia kura 19
hivyo hao wabunge 19 ni kwa ajili ya kuwa mawakala kwenye vituo vya kupigia
kura,” aliongeza
Bangababo alisema ameamua kuchukua fomu ya kugombea nafasi
hiyo ili kuwatumikia wananchi ikiwa ni pamoja na kutatua kero ya wanafunzi wa
Shule ya Sekondari Kizota ya kutokuwa na maabara
Awali, Mtendaji Kata ya Kizota, Loyce Mrefu alisema
wawakilishi wote wa vyama sita waliochukua fomu kwa nafasi hiyo ya udiwani
walirejesha
Waliorudisha fomu ni Jamali Ngalya (CCM), Salum Salum (CUF),
Omary Bangababo (Chadema), Jacklin Msajila (UPDP), Aziz Abbas (NCCR- Mageuzi)
na Peter Malya (NLD).
Wakati hayo yakiendelea Kizota, rufaa ya mgombea ubunge wa Korogwe
Vijijini (Chadema), Asia Saguti aliyeiwasilisha juzi kwa msimamizi wa uchaguzi
imepokewa
Saguti pamoja na viongozi wa Chadema wamekata rufaa NEC
wakipinga kutokupokewa kwa fomu za kugombea
Alipoulizwa jana kuhusu rufaa hiyo, Mkurugenzi wa Uchaguzi
wa NEC, Dk Athumani Kihamia alisema, “NEC inaendelea na taratibu zake na
hatuwezi kujibizana na vyama au chama kimojakimoja katika vyombo vya habari,
tutakapokamilisha, tutatoa taarifa ya pamoja.”
Vyama vinane ambavyo wagombea wake wamepitishwa katika Jimbo
la Monduli vimeanza kampeni huku mchuano mkali ukitarajiwa kuwa kati CCM na
Chadema sanjari na Ukonga
Mchuano huo utakuwa mkali zaidi baada ya ACT Wazalendo
kushirikiana na Chadema na kuwaachia kusimamisha wagombea kwenye majimbo hayo
Mwenyekiti wa Uchaguzi wa ACT Wazalendo, Mohamed Babu
alisema jana kwamba wanatarajia kuzindua kampeni za udiwani katika kata 10 kati
ya 23 zinazorudia uchaguzi
Kuhusu kushirikiana na Chadema, Babu alisema, “Mazungumzo
yanaendelea na yanavyoelekea, tutawaachia wenzetu Chadema Monduli na Ukonga na
wao watatuachia katika hizo kata 10.”
Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje wa
Chadema, John Mrema alisema vikao vya uzinduzi vinaendelea chini ya mwenyekiti
wa kampeni wa Jimbo la Ukonga, Frederick Sumaye ambaye pia ni waziri mkuu
mstaafu
Mrema alisema Monduli ambako aliyewahi kuwa waziri mkuu,
Edward Lowassa ataongoza timu ya kampeni lakini hawajajua watazindua lini,
“Ukonga tutazindua kampeni zetu Jumamosi (kesho) katika viwanja vya
Mzambarauni.”
Kwa upande wake, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Dar es Salaam,
Kate Kamba alisema, “Ratiba bado haijatoka.”
Alipoelezwa kwa mujibu wa ratiba ya NEC, tayari kampeni
zimekwisha kuanza, Kamba alisema, “Hilo unasema wewe, lakini hatujakaa vikao,
labda nitafute kesho (leo) au keshokutwa (kesho).
Jimbo la Monduli ofisa uchaguzi Meleji Kuresoi alisema NEC
imetoa ratiba kwa vyama vyote na “tayari vyama vyote vimeridhia na kuanza
kampeni.”
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Loota Sanare alitamba kuwa
tayari chama chake kimeshinda uchaguzi huo kwani kinakubalika Monduli, jimbo
ambalo liliongozwa na Lowassa miaka 20 kuanzia 1995 hadi 2015.
“Monduli wamejua
makosa waliyofanya sasa wameona kazi nzuri za Serikali na wanaiunga mkono”
alisema Sanare
Mwenyekiti wa Chadema Mkoa Arusha, Aman Golugwa alitaka
uchaguzi uwe huru na haki na wana uhakika wa ushindi asubuhi
Wabunge 19 Chadema kulinda kura za uchaguzi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 24, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment