Dc Longido "Tutazifuta NGO's Zote ambazo hazifanyi kazi yeyote na Zinazojingiza Kwenye Siasa"

Mashirikia yasiyokuwa ya Kiserikali (NGO’s) yametakiwa kutokuwa chanzo cha Migogoro ya Kisiasa kwa wananchi bali yasimamie Sheria na Taratibu zinazowaongoza kwa kufuata makubaliano yaliyofanya na serikali pamoja na kutambuliwa rasmi kwa ajili ya kushirikiana na wananchi

Wilaya ya Longido ina mashirika yasiyo ya kiserikali zaidi ya 30 ambayo yote yamesajiliwa na serikali kwa ajili ya kushirikiana na wananchi.

Hayo yametanabaishwa na Mkuu wa wilaya ya Longido Mkoani Arusha Bwana Frank Mwaisumbe wakati alipokutana na Wasimamizi wa mashirika yasiyokuwa ya kiserikali (NGO’S) zaidi ya 30 ili kuyatambua pamoja na shughuli zinazofanywa na mashirika hayo

Amesema kuwa baadhi ya mashirika yamekuwa chanzo kikubwa cha migogoro kwa wananchi kwa kujingiza katika siasa na kusahau lengo la kazi walizojisajili katika kuwatumikia wananchi husika.

Mwaisumbe amesema kuwa serikali inapenda kushirikiana na mashirika hayo hasa pale yanapofuata utaratibu na sheria zilizoelekezwa na serikali bila kuvunja utaratibu uliopo katika miongozo inayowaelekeza.

Ameongeza kuwa hapendi kusikia shirika lolote limefutiwa usajili kwasababu miongozo inawaelekeza shughuli zao wanazotakiwa kuzitekeleza bila kuathiri wananchi pale wanapotekeleza majukumu yao.

Kwa upande msaidizi wa meneja mradi wa kuwekeza kwa wanawake wa Kimasai Esther Elias Laly amemshukuru mkuu wa wilaya kwa kukaa pamoja na mashirika hayo kwa kuwa lazima kuwepo kwa mahusiano baona yao na serikali.

Ameongeza kuwa kinachotakiwa kwa mashirika hayo kutimiza masharti yaliyowekwa na serikali ikiwemo kulipa kodi pamoja na kujiepusha na siasa kwa kuwa nyingine zinajitokeza kipindi cha siasa pekee.

Kwa upande wa Esuphati Ngorupa amesema kuwa kila shirika lifuate utaratibu waliojiwekea ili lisipelekee kufutiwa usajili kwa kuwa wameaminiwa na serikali ili washirikiane kuletea wananchi maendeleo.

Dc Longido "Tutazifuta NGO's Zote ambazo hazifanyi kazi yeyote na Zinazojingiza Kwenye Siasa" Dc Longido "Tutazifuta  NGO's Zote ambazo hazifanyi kazi yeyote na Zinazojingiza Kwenye Siasa" Reviewed by KUSAGANEWS on August 24, 2018 Rating: 5

No comments: