Miili ya watu watatu yatupwa barabarani Songwe


Miili ya watu watatu imetupwa kando kando ya barabara Kijiji cha Patamela kata ya Saza, wilayani Songwe mkoani hapa, ikiwa na majeraha kichwani

Mkuu wa wilaya hiyo, Samwel Jeremiah ameagiza kufanyika kwa uchunguzi wa haraka ili kubaini chanzo na waliohusika. Amesema hata hivyo miili hiyo bado haijatambulika

“Kweli tukio hilo limetokea na nimeagiza vyombo vyangu vya ulinzi na usalama kufanya uchunguzi wa haraka ili kuwabaini wahusika na tunaomba wananchi wawe watulivu kwa kipindi hiki ambacho tunafanya uchunguzi,” amesema

Shuhuda wa tukio hilo Emmaul Francis, amesema alibaini miili hiyo leo asubuhi akiwa njiani kuelekea kwenye shughuli zake

“Nikiwa njiani kuelekea kwenye shughuli zangu nimekuta mwili wa mtu ukiwa umelazwa kando ya barabara na baada ya kuona hivyo nikawataarifu watu walio karibu na eneo hilo na baada ya kuja tukaona miili mingine miwili ikiwa chini ya karavati ikiwa na majeraha kichwani,” amesema

Francis amesema baada ya kuona miili hiyo walitoa taarifa kituo cha polisi Mkwajuni na baadaye miili hiyo ilichukuliwa na kupelekwa Hospitali ya Mwambani-Songwe

Mganga mkuu wa wilaya ya Songwe, Dk Ibrahim Isack amesema maiti hizo zote ni za kiume na zimeonekana kuwa na majeraha shingoni na kichwani

“Sisi watalaamu tunasubiri polisi wafanye uchunguzi wao ili na sisi tuchunguze kiutalaamu zaidi na baadaye tutaruhusu watu kuja kuitambua,”amesema Dk Isack

Miili ya watu watatu yatupwa barabarani Songwe Miili ya watu watatu yatupwa barabarani Songwe Reviewed by KUSAGANEWS on August 24, 2018 Rating: 5

No comments: