Naibu Rais wa Kenya, William Ruto ametajwa kuwa mwanasiasa
anayeongoza kwa vitendo vya rushwa ikiwa ni maoni yaliyotolewa na wananchi
waliohojiwa kwenye utafiti uliofanywa na taasisi ya utafiti ya Ipsos Synovate
ambayo yanabainisha kwamba asilimia 33 ya Wakenya wanasema anasifika zaidi kwa
vitendo hivyo akifuatiwa na Gavana wa Kirinyaga, Anne Waiguru mwenye asilimia
31
Utafiti huo ulifanywa katika kaunti 45 kwa kuhusisha
washiriki 2,000
Matokeo yanaonyesha asilimia 51 ya Wakenya wana imani na
namna Rais Uhuru Kenyatta anavyopambana kudhibiti vitendo vya rushwa huku
asilimia 32 wakiitaja rushwa kwamba ni tatizo sugu kwa Taifa hilo
Ruto, Waiguru wajibu
Akijibu tuhuma hizo, msemaji wa makamu wa Rais, David
Mugonyi alisema utafiti huo umefadhiliwa na baadhi ya wanasiasa ukilenga
kumchafua bosi wake kuelekea Uchaguzi Mkuu wa 2022
“Wapo wanasiasa wanaoamini wanaweza kufanikiwa kwa mbinu
chafu kama hizi za kuchafuana na kumzuia Ruto ashindwe kugombea urais kama
anavyotarajia. Matokeo ya utafiti hayaonyeshi uhalisia, unapimaje mtazamo wa
watu?” alihoji msemaji huyo
Kuthibitisha mtazamo wake, alisema hata takwimu
zilizowasilishwa zimekaa kisiasa hivyo kuwa vigumu kwa mtu wa kawaida kuziamini
“Katika kipindi ambacho watu wanawaza kubadili Katiba
kumzuia makamu wa rais kugombea nafasi ya juu zaidi haishangazi yanapotolewa
matokeo ya utafiti kama huu,” alisisitiza
Msemaji huyo hakuwa peke yake kupinga utafiti huo, Waiguru
pia alisema hajawahi kufikishwa mahakamani kwa tuhuma yoyote inayohusiana na
rushwa hivyo akashangazwa na kuwekwa juu katika utafiti huo
“Ipsos inatumika kisiasa kuwachafua baadhi ya watu hasa
wanaoogopwa kwenye Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2022. Wameona Kaunti ya
Kirinyaga inasonga kimaendeleo na wanahaha,” alisema Waiguru
Licha ya Ruto na Waiguru, kwenye orodha hiyo pia yumo Aden
Duale, kiongozi wa wengi katika Bunge la Kitaifa ambaye amepigiwa kura nyingi
na wananchi walioshiriki utafiti huo
“Tuhuma za rushwa hazitakiwi kupimwa kwa maoni ya mtu, bali
ushahidi. Huwezi kuwatuhumu watu kwa maoni ya mamluki,” alisema Duale
Utafiti wamtaja Makamu Rais Kenya kuongoza kwa rushwa
Reviewed by KUSAGANEWS
on
August 23, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment